Header AD

MKONGWE RIO FERDINAND AMPIGIA PANDE VAN GAAL MAN UNITED, ASEMA JAMAA ANAFAA KINOMA!


 Van Gaal the right personality for Manchester United, says Rio Ferdinand
BEKI mkongwe wa Manchester United, Rio Ferdinand anaamini Louis van Gaal ni mtu sahihi kukabidhiwa majukumu ya ukocha mkuu klabuni hapo.
Kutangazwa kwa Mholanzi huyo kama mirthi wa David Moyes kulistishwa jana alhamisi ili kumuacha huru wakati huu akiiandaa timu ya taifa ya Uholanzi kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Ecuador.
Van Gaal amewahi kuongeza klabu kubwa za dunia, hivyo  beki huyo wa kati ambaye hatakuwepo Old Trafford msimu ujao baada ya kutangaza kuondoka majira ya kiangazi mwaka huu amesema kocha huyo anaweza kuleta mafanikio katika michuano ya ligi kuu.
“Anaonekana mtu imara sana na muelekezaji. Ana uelewa na ufahamu mkubwa kwa kila anachotaka kufanya. Unatakiwa kuwa hivyo katika klabu kama Man United,” Ferdinand aliwaambia waandishi wa habari.
MKONGWE RIO FERDINAND AMPIGIA PANDE VAN GAAL MAN UNITED, ASEMA JAMAA ANAFAA KINOMA! MKONGWE RIO FERDINAND AMPIGIA PANDE VAN GAAL MAN UNITED, ASEMA JAMAA ANAFAA KINOMA! Reviewed by crispaseve on 02:37 Rating: 5

No comments

Post AD