Header AD

IRINGA WAADHIMISHA SIKU YA MASHUJAA

 ??????????????????????
Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Kilolo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Gerald Guninita akiweka ngao ya jadi katika sehemu inayotarajiwa kujengwa Mnara wa Mashujaa wa Jeshi la Mkwawa waliopigana vita dhidi ya dhuluma za Wajerumani, Mnara huo upo karibu na walipozikwa askari wa kijerumani 300 wakati wa vita na chifu wa wahehe Chifu Mkwawa mnamo mwaka 1891 wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yaliofanyika kimkoa katika Kijiji cha Lugalo wilayani Kilolo mkoani Iringa.
1
Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakipita kwa gwaride la heshima katika maadhimisho ya siku ya mashujaa yaliofanyika kimkoa katika Kijiji cha Lugalo wilayani Kilolo mkani Iringa leo.
3
Mkuu wa wilaya ya Kilolo Gerald Guninita(Kushoto) akiwa pamoja na mwenyekit wa Halmashauri ya wilaya hiyo
Joseph Muhumba wakitoa heshima  wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yaliofanyika kimkoa katika Kijiji cha Lugalo wilayani Kilolo.
5
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya,Pudenciana Kisaka (mwenye pinki) sambamba na wakuu wa wilaya ya Mufindi na Iringa wakitoa heshima wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yaliofanyika kimkoa katika Kijiji cha Lugalo wilayani Kilolo.
??????????????????????
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa ACP, Ramadhani Mungi akiweka silaha ya jadi (mkuki) kwenye mnara wa mfano wa mashujaa. Mnara wa mashujaa wa askari wa Chifu Mkwawa utarajia kujengwa mahali hapo karibu na mnara wa wajerumani 300 waliozikwa katika Kijiji cha Lugalo wilayani Kilolo, Mkoa wa Iringa.
9
Baadhi ya wananchi waliohudhuria maadhimisho hayo. (Picha zote na Denis Mlowe)
IRINGA WAADHIMISHA SIKU YA MASHUJAA IRINGA WAADHIMISHA SIKU YA MASHUJAA Reviewed by crispaseve on 02:48 Rating: 5

No comments

Post AD