Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga, amekanusha vikali uvumi uliosambaa kwenye mitandao ya kijamii mapema leo, kuwa Sitti Abbas Mtemvu amelazimika kuvua taji la Uremo la Tanzania (Redd’s Miss Tanzania 2014).
Sehemu ya Taarifas inayosadikiwa kuwa ni ya uvumi iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii mapema leo
MKURUGENZI wa Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga
Redd’s Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu
-
MKURUGENZI wa Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga,
amekanusha uvumi uliosambaa kwenye mitandao ya kijamii mapema leo, kuwa
Sitti Abbas Mtemvu amelazimika kuvua taji la Uremo la
Tanzania (Redd’s Miss Tanzania 2014). Uvumi wa Sitti kuvua taji hilo
umetokana na taarifa zilizotolewa kupitia akaunti ya Facebook mrembo
huyo anayelalamikiwa kughushi vyeti vya kuzaliwa, akisema kutokana na
vidole vya lawama anavyooshewa kiasi cha kuosa amani, amelazimika
kuvua taji ili awe huru.
“Habari za jioni Watanzania wenzangu, kutokana
na kuwa nimekuwa nikisemwa sana, maneno mengi yasio na tija juu ya hili
taji la U-Miss anzania 2014,,mpaka kupelekea nisiwe na amani na uhuru
ndani ya nchi yangu Tanzania, kwa roho safi nimeamua mwenyewe kujivua
taji hilo na kuacha wanaye ona anastahili taji hili apewe ili niendelee
na maisha yangu kwa amani ,isiwe shida sana kwani sitegemei taji hili
ili kuishi!!” imeandikwa katika ukurasa huo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga, amekanusha vikali uvumi uliosambaa kwenye mitandao ya kijamii mapema leo, kuwa Sitti Abbas Mtemvu amelazimika kuvua taji la Uremo la Tanzania (Redd’s Miss Tanzania 2014).
Reviewed by crispaseve
on
09:13
Rating:
Post a Comment