Header AD

SHULE YA WALEMAVU BUHANGIJA JUMUISHI YAELEMEWA NA CHANGAMOTO

DSC_0162
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akimsikiliza kwa makini Mkuu wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi aliyekuwa akimwelezea changamoto mbalimbali walizonazo shuleni hapo.(Picha na Zainul Mzige).

Na MOblog, Shinyanga
SHULE ya watoto wenye ulemavu ya Buhangija Jumuishi inakabiliwa na changamoto kubwa zinazofanya maisha kwa watoto hao kuwa magumu. Miongoni mwa changamoto hizo ni kukosekana kwa huduma za matibabu, walimu wa kutosha na mabweni.

Hayo yamebainika wakati wa ziara fupi ya Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues. Mkuu wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi iliyopo mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi, ndiye aliyeelezea ugumu uliopo katika shule hiyo yenye wanafunzi 209 wenye ulemavu wa aina mbalimbali.
DSC_0173
Mkuu wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi akimtambulisha Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyefanyia ziara fupi akiwa safarini kuelekea jijini Mwanza akiwa ameambatana na Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias (katikati).

Alisema shule hiyo yenye walemavu wa aina tatu wa kusikia, ngozi na wasioona inakabiliwa pia na lishe duni ambayo haimpi kijana nafasi ya kuendelea, kwani wanakula mlo wa aina moja na kidogo. Shule hiyo ambayo awali ilikuwa inawapokea wanafunzi wasioona sasa inapokea walemavu wa ngozi kutokana na hofu iliyokuwa inalikumba taifa ya mauaji ya albino.

Aidha mwalimu huyo alisema kwamba wameiomba serikali kuwa na muuguzi na daktari katika makazi hayo lakini mpaka sasa hawajapatiwa kutokana na wao wenyewe kutokuwa na uwezo wa kuwalipa. Alisema kutokana na rika mbalimbali na tatizo la walemavu wa ngozi shule hiyo ambayo sasa imegeuzwa kuwa makazi inastahili kuwa na daktari na mabweni yaongezwe.
SHULE YA WALEMAVU BUHANGIJA JUMUISHI YAELEMEWA NA CHANGAMOTO SHULE YA WALEMAVU BUHANGIJA JUMUISHI YAELEMEWA NA CHANGAMOTO Reviewed by crispaseve on 07:02 Rating: 5

No comments

Post AD