Header AD

Mkopo kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Vijana wakomboa Kikundi cha Iringa Promise Keepers

Afisa Maendeleo ya Vijana Wilaya ya Chamwino Bw. Denis Vagela (kushoto) akizungumza na Vijana wa kikundi cha Wajasiriamali wa Wilaya ya Chamwino wanaojishughulisha na utengenezaji wa Sabuni za maji, Batiki na ufundi walipotembelewa kwa ajili ya kuangalia mradi wao leo Mkoani Dodoma. Katikati ni Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa, na aliyekaa ni Afisa Vijana Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga.
Wakwanza mbele ni Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa akiangalia mashine ya kukamua alizeti iliyotengenezwa na Vijana wa kikundi cha Chachu ya Maendeleo Dodoma wakati wa kutembelea miradi ya vijana wa Mkoa wa Dodoma. Kulia ni kijana wa kikundi hicho Bw. Ayoub Athumani.
Kijana Samwel Nagija kutoka kikundi cha vijana cha Chachu ya Maendeleo Dodoma kinachojishughulisha na utengenezaji wa mashine za kusaga na kukoboa, mashine za kutengeneza matofali, mashine za kukamua alizeti, na ujenzi wa vitanda na madawati ya chuma akiendelea na ujenzi wa mashine ya kusaga leo Mkoani Dodoma.
Mwenyekiti wa kikundi cha vijana cha Iringa Promise Keepers Bw. Rashid Magule (kushoto) kinachojishughulisha na ufundi Selemala akielezea namna kikundi chake kilivyofaidika na mkopo unaotolewa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana. Wanaomsikiliza kutoka kulia ni Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa, anayefuata ni Afisa Maendeleo ya Vijana Bi. Amina Sanga na wapili kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw.Laurean Masele. (Picha na Genofeva Matemu – Maelezo, Dodoma)
Mkopo kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Vijana wakomboa Kikundi cha Iringa Promise Keepers Mkopo kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Vijana wakomboa Kikundi cha Iringa Promise Keepers Reviewed by crispaseve on 10:23 Rating: 5

No comments

Post AD