Bilioni 43.89 zatumika kusambaza umeme Dodoma

Na Greyson Mwase, Dodoma
Meneja
wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco)
mkoa wa Dodoma, Zakayo Temu amesema kuwa Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 43.89 kwa ajili ya kujenga miundombinu
ya umeme katika mkoa wa Dodoma kupitia
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili.
Temu
aliyasema hayo mbele ya Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Nishati na Madini
iliyopo mkoani Dodoma kwa ajili ya kukagua miradi ya umeme
ili kujionea utekelezwaji wake pamoja na kuzungumza na wawakilishi wa
wananchi. Mbali na mkoa wa Dodoma, kamati hiyo
inatarajia kufanya ziara ya kukagua miradi ya umeme katika mikoa ya Singida, Arusha na Kilimanjaro pamoja na kuzungumza na wadau wa madini katika mkoa wa
Manyara.
Akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya umeme
katika mkoa wa Dodoma chini ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili, Temu alisema kuwa mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini
awamu ya pili unahusisha
wilaya zote za mkoa wa Dodoma, wilaya za
Chamwino, Kongwa zikiwa mojawapo.
Akielezea
kazi ya usambazaji wa umeme katika wilaya
ya Chamwino Temu alisema kazi ya
kupeleka umeme itahusisha ujenzi wa njia
ya umeme msongo wa kilovolti 33 urefu wa kilomita 171.5 na njia ya msongo wa kilovoti 0.4 urefu wa kilomita 95.
Alisema ujenzi utahusisha pia ufungaji wa transfoma
22 za ukubwa mbalimbali pamoja na
kuunganisha wateja wapatao 1,195 kwa gharama inayokadiriwa kuwa shilingi za
kitanzania bilioni 8.67.
Aliongeza
kuwa katika wilaya ya Chamwino hadi sasa ujenzi wa miundombinu ya umeme
umefikia asilimia 52 na wateja 105 kati ya 1,195 wamekwisha unganishwa
na huduma ya umeme na kusisitiza kuwa
mradi huu unatarajiwa kukamilika
mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
Bilioni 43.89 zatumika kusambaza umeme Dodoma
Reviewed by crispaseve
on
07:34
Rating:

Post a Comment