Airtel na VETA yatoa elimu juu ya masomo ya ufundi kupitia simu ya VSOMO
Walimu na wanafunzi wa
Chuo cha VETA Kipawa wakimsikiliza Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson
Mmbando (kushoto) akifafanua juu ya ushirika kati ya Airtel na VETA kwa
kuleta mafunzo ya ufundi stadi kutoka VETA
kwa njia ya simu yajulikanayo kama Vsomo yaani VETA Somo, katika semina
iliyofanyika chuoni hapo Kipawa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki
iliyopita.
Mkuu wa Chuo cha VETA
Kipawa, Eng. Lucius Lutenganya akifafanua jambo kwa walimu na wanafunzi
wa chuo hicho juu ya programu ya Vsomo yaani VETA Somo inayotolewa na
kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel ambapo
wanafunzi wa Chuo cha VETA watapata fursa ya kusoma kupitia simu za
mkononi, kulia ni Meneja huduma kwa Jamii wa Airtel Hawa Bayumi na
Mratibu wa kozi fupi na ujasiriamali VETA kipawa, Gosbert Kakiziba.
Semina hiyo
iliyofanyika chuoni hapo Kipawa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.
Meneja huduma kwa
Jamii wa Airtel Hawa Bayumi (kulia) akielezea faida za programu ya VSOMO
kwa walimu na wanafunzi wa chuo cha VETA Kipawa inayowezesha kupata
mafunzo ya ufundi stadi kutoka VETA kwa njia ya
simu katika semina iliyofanyika chuoni hapo Kipawa jijini Dar es Salaam
mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mratibu wa kozi fupi
na ujasiriamali VETA kipawa, Gosbert Kakiziba akijibu swali juu ya kozi
zipatikanazo kupitia program ya VSomo yaani VETA Somo inayowezesha
kupata mafunzo ya ufundi stadi kutoka VETA kwa
njia ya simu, katika semina iliyofanyika chuoni hapo Kipawa jijini Dar
es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.
Wanafunzi wa Chuo cha Veta Kipawa wakisikiliza kwa makini katika semina juu ya mpango wa VSomo yaani VETA Somo
inayowezesha kupata mafunzo ya ufundi stadi
kutoka VETA kwa njia ya simu, ambapo wanafunzi wa VETA watapata fursa
ya kusoma kwa kupitia simu za mkononi wakati wa semina iliyofanyika
chuoni hapo Kipawa jijini Dar es Salaam mwishoni
mwa wiki iliyopita
Airtel na VETA yatoa elimu juu ya masomo ya ufundi kupitia simu ya VSOMO
Reviewed by crispaseve
on
01:50
Rating:
Post a Comment