TASISI YA KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA (THPS) YAANDAA MKUTANO WA SIKU MOJA WA WADAU WA MAPAMBANO YA VVU NA UKIMWI ZANZIBAR
Waziri
 wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akifungua mkutano wa wadau wa mapambano ya
 ukimwi Zanzibar katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni.

Waziri
 wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akizindua Mpango Mkakati wa miaka mitano 
wa THPS katika mkutano wa wadau wa mapambano ya ukimwi uliofanyika 
Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni, anaeshirikiana nae katika 
uzinduzi huo ni Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Redempta Mbatia.

Mkurugenzi
 Mtendaji wa THPS Dkt. Redempta Mbatia akizungumza na wadau wa mapambano
 ya ukimwi Zanzibar katika mkutano wa siku moja uliofanyika Hoteli ya 
Zanzibar Beach Resort Mbweni.

Muhudumu
 Mkuu wa huduma za mama na mtoto na huduma za upimaji vvu kwa jamii 
kutoka Hospitali ya Mwembeladu Mwanakhamis Alawi Nguzo akipokea zawadi 
maalum kutoka Waziri wa afya Mh. Thabit Kombo baada ya kuwa kituo bora 
katika mapambano ya ukimwi kipindi cha miezi mitatu Octoba – Disemba.

Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya kuimarisha huduma za afya Tanzania (THPS) Dkt. 
Redempta Mbatia akimkaribisha Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo 
alipowasili kufungua mkutano wa wadau wa mapambano ya ukimwi Hoteli ya 
Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Na Ramadhani Ali-Maelezo
Taasisi
 zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya 
ukimwi (VVU) na ukimwi Zanzibar zimetakiwa kuelekeza nguvu katika 
makundi maalum ambayo maambukizi bado ni makubwa.
Waziri
 wa Afya Mahmoud Thabit Kombo alitoa ushauri hao alipokuwa akifungua 
mkutano wa siku moja wa wadau wa mapambano ya ukimwi uliotayarishwa na 
Taasisi ya kuimarisha huduma za afya Tanzania (THPS) na kuzindua mpango 
mkakati wa miaka mitano wa taasisi hiyo katika Hoteli ya Zanzibar Beach 
Resort Mbweni.
Alisema
 wakati Zanzibar inajivunia kuwa na asilimia chini ya moja ya maambukizi
 ya VVU, katika makundi maalumu maamukizi yapo kwa asilimia 10 hadi 19 
ambapo ni hatari.
Aliyataja
 makundi hayo kuwa ni vijana wanaojidunga sindano za madawa ya kulevya, 
wanawake wanaofanya biashara ya ngono na wanaume wanaofanya ngono na 
wanaume wenzao.
Alisema kunapokuwa na kikundi kidogo cha watu wenye hali kubwa ya maambukizi ya VVU hatari ya maambukizi inaelekea kwenye jamii.
“Makundi
 maalum yanaonekana kuwa ni daraja la maambukizi ya Virusi vya Ukimwi 
kutoka kwao kuja kwenye jamii, ”alisisitiza Waziri wa Afya.
Aliongeza
 kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeridhia kuyafanyia kazi malengo 
ya dunia ya kutokomeza kabisa maambukizi ya VVU ifikapo mwaka 2030 hivyo
 mashirikiano zaidi yanahitajika katika kufikia malengo hayo.
Hata 
hivyo alieleza kuwa ushiriki wa wananchi katika kupima VVU bado 
hauridhishi na wale wanaopima na kubainika na maambukizi wengi wao 
hawajiungi kwenye huduma za tiba na wachache wanaotumia dawa hawazitumii
 ipasavyo.
Waziri
 wa Afya alikumbusha kuwa wakati huu ambapo Zanzaibar inatekeleza Mpango
 wa kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa 
ujauzito lakini wanaume hawajitokezi kupima afya zao.
“Akinababa
 tuwasindikize wake zetu kliniki ili na sisi tupimwe Virusi vya ukimwi, 
hivi sasa tupo chini ya asilimia tano wakati wenzetu Tanzania Bara 
wamefikia asilia 80, “Waziri Mahmoud alihimiza.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa THPS Dkt. Redempta Mbatia alisema katika kupambana na 
ukimwi Zanzibar, taasisi hiyo imekuwa ikiwajengea uwezo wafanyakazi wa 
afya na taasisi nyengine zinazoshiriki katika mapambano hayo.
Aidha 
alisema wamekuwa wakisaidia masuala ya uongozi pamoja kuimarisha utawala
 bora na kusaidia vifaa tiba katika Hospitali na vituo vya afya ili 
kuhakikisha huduma za afya zinakuwa endelevu na kufikia malengo 
yaliyowekwa.
TASISI YA KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA (THPS) YAANDAA MKUTANO WA SIKU MOJA WA WADAU WA MAPAMBANO YA VVU NA UKIMWI ZANZIBAR
 
                    Reviewed by crispaseve
                    on 
                    
10:56
 
                    Rating: 
                    
 
                    Reviewed by crispaseve
                    on 
                    
10:56
 
                    Rating: 



Post a Comment