MKURUGENZI MKUU MSD AFANYA ZIARA HOSPITALI JIJINI DAR ES SALAAM
 Mkurugenzi
 Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu (kushoto), akizungumza 
na viongozi mbalimbali wa Hospitali ya Sinza alipofanya  ziara ya kikazi
 katika Hospitali hiyo na  Mwananyamala jijini Dar es Salaam leo, ili 
kubaini changamoto zilizopo za  upatikanaji wa dawa na vifaa tiba na 
kuzipatia ufumbuzi wa pamoja. Kutoka kulia ni Meneja wa MSD Kanda ya Dar
 es Salaam, Celestine Haule na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Sinza, 
Chrispin Kayola.
 Maofisa wa Hospitali ya Sinza wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu (hayupo pichani)
 Mkutano ukiendelea.
  Mganga Mkuu wa Hospitali ya Sinza, Chrispin Kayola, akizungumza katika mkutano huo.
 Laboratory Manager wa Hospitali ya Sinza, Emmanuel Kiponda, akichangia jambo kwenye mkutano huo.
 Meneja wa MSD Kanda ya Dar es Salaam, Celestine Haule, akizungumza kwenye mkutano huo.
 Mkurugenzi
 Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu, akiwa katika picha ya 
pamoja na maofisa wa Hospitali ya Sinza baada ya kufanya nao mazungumzo.
Mkurugenzi
 Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu, akiwa katika picha ya 
pamoja na maofisa mbalimbali wa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala.
Na Dotto Mwaibale
MKURUGENZI
 Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu amewatembelea wateja wa
 MSD wanaohudumiwa na Kanda ya MSD Dar e's Salaam ukiwa ni pamoja na 
Hospitali ya Mwananyamala na Sinza kubaini changamoto zilizopo katika 
upatikanaji wa dawa na vifaa tiba ili kuzipatia ufumbuzi.
Katika
 ziara hiyo iliyofanyika jumanne jijini Dar es Salaam Bwanakunu 
amewataka wateja hao kufanya Maoteo ya mahitaji yao sahihi na 
kuyawasilisha Msd kwa wakati kwa mujibu wa sheria yaani tarehe 30 
Januari kila mwaka,hasa dawa na vifaa tiba vinavyonunuliwa kwa Manunuzi 
maalumu.
Bwanakunu
 alihimiza watoa huduma katika hospitali hizo kutambua jukumu walilonalo
 katika usimamizi wa matumizi ya dawa na vifaa tiba kwa wananchi.
Akizungumza
 akiwa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala Bwanakunu alisema anazitambua 
changamoto zilizopo za usambaji wa dawa na vifaa tiba na wamedata msaada
 wa magari kutoka Global Fund ambayo yataboresha usambazaji kutoka mara 
nne kwa mwaka hadi mara sita kwa mwaka.
Kuhusu
 vifaa vya Manunuzi maalumu Bwanakunu amesema hospitali zikiwa zinaomba 
kwa wakati mmoja ingerahisisha kuagiza vifaa hivyo mapema,badala ya kila
 hospitali kuleta kwa wakati wake.
"Vifaa hivi tunaagiza nje ya nchi na mchakato wake unachukua muda mrefu na changamoto kubwa " alisema Bwanakunu.
Mganga
 Mkuu wa Hospitali ya Sinza, Chrispin Kayola alisema hali ya upatikanaji
 wa dawa na vifaa tiba katika hospitali hiyo kwa sasa ni asilimia  80 .
"Changamoto
 iliyopo ni uhaba wa vitendanishi vya maabara na vifaa vya macho na meno
 ambavyo tunapata chini ya kiwango hivyo havikidhi mahitaji tuliyonayo,"
 alisema.
Kwa
 upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, 
Daniel Mkungu alisisitiza haja ya ushirikiano baina ya Hospitali hizo na
 MSD ili kuboresha huduma za afya hapa nchini.
Ziara hiyo ya mkurugenzi huyo itaendelea tena kesho katika baadhi ya hospitali zilizopo jijini Dar es Salaam.
MKURUGENZI MKUU MSD AFANYA ZIARA HOSPITALI JIJINI DAR ES SALAAM
 
                    Reviewed by crispaseve
                    on 
                    
14:56
 
                    Rating: 
                    
Post a Comment