MWANRI AAGIZA WATOTO WASIPORIPOTI SHULE WAZAZI WAO WAKAMATWE
SERIKALI
 Mkoani Tabora imeagiza kukamatwa mara moja wazazi au walezi ambao hadi 
kufikia Jumatatu ijayo (15, January 2018) watakuwa wameshindwa 
kuhakikisha kuwa watoto wao waliochaguliwa kujiunga Kidato cha kwanza 
mwaka huu watakuwa hajaripoti katika Shule walizopangiwa.
Agizo
 hilo limetolewa jana mjini Sikonge na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey 
Mwanri baada ya kupata taarifa kutoka kwa Afisa Elimu Mkoa iliyoakuwa 
ikionyesha kuwa idadi kubwa ya wanafunzi walichaguliwa kujiunga na 
Kidato cha kwanza mwaka 2018 bado wengi wao hawajaripoti katika Shule 
walizopangiwa.
Alisema
 kuwa kufikia Jumatatu ijayo anataka kupata taarifa na majina ya 
wanafunzi wote waliochangiwa ambao hawako shuleni ikiwa  na majina ya 
wazazi wao ili hatua za kisheria dhidi yao ziweze kuchukuliwa kwa kosa 
la kumkoshesha watoto haki ya kupata elimu.
Mwanri
 aliongeza kuwa viongozi wa kuanzia mitaa, vitongoji, vijiji , Kata na 
Wilaya ni vema wahakikishe wanawatafuta watoto wote waliochaguliwa ambao
 hawako shuleni ili kujua walipo na wanafanya nini kwa kuwa inawezekana 
wapo ambao tayari wameshaozeshwa.
Alisisitiza
 kuwa wakikuta mtoto yupo nyumbani na mzazi wake hataki kumpeleka Shule 
wamukamate mzazi wake ili hawawezi kuwajibika kwa uzembe wake.
“Hapa
 tutakwenda kwa Sera ya mbanano…kama kiongozi lazima umbane mzazi ambaye
 hadi hivi sasa hajampeleka mtoto shule wakati wenzake wameshaanza 
masomo na ikibidi mfikisheni katika vyombo vya Sheria ili ajibu 
mashitaka yake ya kunyima mtoto haki yake ya elima”alisema Mkuu huyo wa 
Mkoa wa Tabora
Akitoa
 taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora wakati wa ziara ya kukagua zoezi la 
upandaji miti kwa ngazi ya Shule za Msingi na Sekondari ,Katibu Tawala 
Msaidizi (Elimu) Suzan Nussu alisema kuwa hali ya watoto kuripoti katika
 Shule za Sekondari kwa wanafunzi walichaguliwa kujiunga na Kidato cha 
Kwanza mwaka huu bado sio nzuri kwa baadhi yao hawajafika shuleni hadi 
hivi sasa.
Alisema
 kuwa katika Shule ya Sekondari ya Ngulu iliyopo Sikonge walichaguliwa 
watoto 130 lakini hadi hivi sasa wamejiunga 44, Shule ya Sekondari 
Usisya iliyopo Urambo wamechaguliwa 130 lakini waliripoti ni 54 na Shule
 ya Sekondari Nanga Sekondari iliyopo Igunga waliochaguliwa ni 160 
lakini walioripoti ni 7 hadi kufikia sasa.
Nussu
 alisema kuwa kuchelewa kuripoti kwa wanafunzi hao sio tu kunarudisha 
nyuma maendeleo ya watoto hao kwa sababu ya kuachwa na wenzao bali pia 
kunasababisha usumbufu kwa walimu kuanza upya kuwafundisha wanafunzi 
waliochelewa ili waweze kwenda na kasi ya wenzao.
Alitoa
 wito kwa wazazi kuhakikisha ifikapo mapema wiki ijayo watoto wote wawe 
wamefika Shule kwani tayari Serikali ilishafuta ada na hivyo hakuna 
kisingizio ambacho kinaweza kumsababisha mtoto kushindwa kuanza masomo 
yake kwa ajili ya faida yake na Taifa kwa ujumla.
Nussu
 alisema kuwa michango mingine inapangwa na wazazi wa watoto wa Shule 
husika kwa kukubaliana na Kamati za Shule na hivyo hakiwezi kuwa kikwazo
 kwa watoto kushindwa kuhudhuria masomo yao.
Kwa
 upande wa Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ngulu  Israel Mwambikwa alisema
 kuwa amekuwa akipata tatizo kutoka kwa baadhi ya wazazi kushindwa kutoa
 hata michango waliokubaliana katika vikao vyao ya kutoa kilo 10 za 
mahindi ,kilo mbili za maharage na shilingi 17,000/- ambazo wazazi 
walikubaliana kama mahitaji ya chakula cha kila mtoto kwa mwezi.
MWANRI AAGIZA WATOTO WASIPORIPOTI SHULE WAZAZI WAO WAKAMATWE
 
                    Reviewed by crispaseve
                    on 
                    
09:11
 
                    Rating: 
                    
 
                    Reviewed by crispaseve
                    on 
                    
09:11
 
                    Rating: 


Post a Comment