Header AD

MKUTANO WA RC RUVUMA NA WANAKIJIJI WA KIJIJI CHA MTUNDUWALO

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akizungumza  leo na wananchi wa kijiji cha Mtunduwalo kata ya Luanda wilaya ya Mbinga kufuatia malalmiko yao ya kulipwa fidia isiyolingana na thamani ya eneo waliloachia kupisha mradi wa mgodi wa Makaa ya Mawe Ngaka.
Picha Na Revocatus Kassimba
Afisa Habari
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma
Mmoja wa wanakijiji Mtunduwalo John Nyimbo akitoa maelezo juu ya malalamiko yao kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma (hayupo pichani) kuhusu kulipwa fidia kidogo ya ardhi waliyoitoa kupisha mradi wa mgodi wa makaa ya mawe Ngaka wilayani Mbinga.
Wananchi wa kijiji cha Mtunduwalo katika Kata ya Luanda wilaya ya Mbinga wakisikiliza kwa makini maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma (hayupo pichani) kuhusu malalamiko ya kulipwa fidia pungufu ya maeneo yao kupisha mradi wa makaa ya mawe Ngaka hivi leo.
 
Mkuu wa Mkoa waRuvuma Said Mwambungu akiagana na wanakijiji cha Mtunduwalo baada ya kumalizika kwa mkutano
Reviewed by crispaseve on 09:59 Rating: 5

No comments

Post AD