BEYONCE AWASHANGAZA MASHABIKI WAKE KWA KUACHIA ALBUM YAKE BUREEE..
Diva anayefanya vizuri katika anga ya muziki wa kimataifa, Beyoncé Giselle Knowles-Carter a.ka Mrs Carter, siku ya jana Desemba 12 alishangaza mashabiki wake Duniani baada ya kuachia album yake ya tano inayokwenda kwa jina la ‘Beyoncé katika application ya Itunes bila ya kuifanyia promo na kutoweka masharti ya aina yoyote, pia Beyonce alifunguka kwa kusema kwamba ”hakujisikia kuachia albamu yake kama jinsi afanyavyo kipindi cha nyuma na pia anao uwezo wa kuongea moja kwa moja na mashabiki wake kwani anaamini kwamba wao ni kiungo kimojawapo katika muziki anaofanya.
Katika albamu hiyo yenye jumla ya nyimbo na video 17 ambapo ndani yake amewashirikisha wasanii wakubwa kama Jay Z, Kelly Rowland, Michelle Williams, Frank Ocean, Pharrell Williams, Justin TimberLake, , Drake na mtoto wake Blue Ivy… Tazama Baadhi ya Video zilizopo katika albamu yake hiyo..
BEYONCE AWASHANGAZA MASHABIKI WAKE KWA KUACHIA ALBUM YAKE BUREEE..
Reviewed by crispaseve
on
21:30
Rating:
Reviewed by crispaseve
on
21:30
Rating:

Post a Comment