SOMA MKASA HUU WA KWELI UNAOSISIMUA NA KUTISHA ILA WENYE MAFUNZO YA KUTOSHA KWETU SISI.
Katika kijiji cha Matare wilaya ya Magumu Serengeti alikuwa
akiishi bwana mmoja aliyeitwa Wambura, siku moja isiyo na jina
alishangaa ghafla akiwa mikononi mwa polisi kwa kesi ya kusingiziwa
kisha kuhukumiwa kwenda jela miaka mitatu.
Huku nyuma akiacha mke na watoto wanne waliokuwa wanasoma.
Hukumu hiyo ilimtesa sana kichwa chake, alitamani kila mtu anayemhisi
anamakosa aingie katika moyo wake na kuupata ukweli. Alilia sana na
umaskini wake, labda angepata wakili mzuri angeweza kumtetea, kitendo
chake cha kumkosa wakili kukahalalisha kifungo hicho.
Alikwenda gerezani huku akiumia sana rohoni. Alianza maisha
mapya kwa shida sana, akawa mnyonge kila wakati na mwili wake ukapoteza
afya kwa ujumla, huko gerezani alifanikiwa kupata rafiki aliyekuwa na
cheocha ama jukumu la uzikaji wa wafungwa hasahasa ambao hawakuwa na
ndugu ama ambao ndugu zao huwa hawajitokezi pale gerezani.
Rafiki wake mpya huyo ambaye alikuwa mzkaji alijaribu sana
kumtia moyo Wambura na kumwaminisha kuwa hiyo ilikuwa hatua tu ya maisha
ivyo anapaswa kukubaliana na hali halisi kwani ipo siku ukweli utakuja
kujulikana. . Bwana Wambura yale maneno ya mzikaji hayakumuingia kabisa
alizidi kunyong’onyea. ‘’Siwezi kuvumilia kukaa gerezani kwa miaka
mitatu… kama unajali kilio change nisaidie nitoroke kwa namna yoyote ile
ndugu yangu’’. Wambura alimsihi mzikaji.
Siku moja mzikaji akamwambia bwana Wambura kuwa msaada
umepatikana. Lakini yataka moyo, ‘’Nipo tayari kwa lolte ili mradi tu
nitoke humu ‘’ alijibu bila kumung’unya huku akimtegea sikio mzikaji .
‘’Msaada pekee wa kukutorosha humu ndani ni kwa njia ya jeneza. Yaani
mfungwa akifa mimi nakuunganisha naye kwenye jeneza ‘’ . akashusha
pumzi kisha akaendelea ‘’wewe ukisikia kengele ya msiba njoo mara moja
kwenye chumba cha maiti utakuta tayari sanduku liko katikati ya chumba
linakuwa halijafungwa, funua mfuniko ingia ndaniyake ulale pembeni ya
maiti kwani sanduku huwa kubwa la kutosha kila aina ya maiti na hata
miili miwili inaingia, kisha nitakuja kulipigilia misumari . Baada ya
muda tutalipakia kwenye gari na kutoka kwenda nje ya gereza makuburini
nikiongozana na baadhi ya wafungwa na maaskari magereza.
Tutakuzika huko lakini baada ya dakika 20 hadi 30 nitarudi
kukufukua. Hautaweza kushindwa kupumua kwa dakika hizo, utatoka ukiwa
huru’’ .
Japokuwa wazo lilikuwa zuri lakini lilimtisha sana Wambura.
Hata hivyo akaona afadhali afanye hivyo kuliko kukaa gerezani miaka
mitatu bila kosa. Siku moja akasikia kengele ya msiba, akafanya kama
alivyoelekezwa na mzikaji. Akaenda kuingia chumba cha maiti, kweli
alikuta sanduku huku akiwa na hofu akaingia na kulala pembeni ya maiti
iliyokuwepo, mara akasikia mtu ameingia na kulipigilia msumari sanduku
muda mfupi baadae sanduku likainuliwa na kuwekwa kwenye gari.
Gari likatoka nje ya gereza hadi makaburini, sanduku
likashushwa na kuwekwa kaburini na kuanza kufukiwa, Wambura alijitaidi
sana kuvumilia japo hofu ilizidi kumtanda, ALIMTEGEMEA SANA MZIKAJI na
alianza kumuona mkombozi wa maisha yake kama alivyoambiwa, akasubiri
dakika kumi, ishirini.. zikapita kimya, Dakika 30 kimya… Joto nalo
likazidi kuongezeka. “Nitavumilia hadi afike’’ alijisemea kisha
akaongezea kauli ya ujasiri ‘’Kama nilitakiwa kuishi miaka mitatu kivipi
dakika kadhaa za hapa kaburini zinishinde” kwa kuwa alishakaa kwenye
jeneza kwa muda kiasi akatamani kujua aliyekufa ni nani.. ni kweli
aliogopa kuitazama maiti lakini aliona kama inatisha zaidi ikiwa
imefunikwa vile kuliko ikiwa wazi.
Akaifunua upande wa usoni kwa kuwa kulikuwa na giza nene
alikodoa sana macho kuitazama. Lahaula macho yakakutana na sura ya
mzikaji alikuwa amekufa na amezikwa na ahadi zake za ukombozi.
FUNZO : Usimtegemee sana mwanadamu katika maisha yako,
kwanza ni dhambi, pili mwanadamu anakumbana na vikwanzo kama
unavyokumbana navyo wewe hadi kumwendea yeye.
Hivyo kumpatia maisha yako ni kuzidi kuyaweka rehani na
hatarini zaidi, kama umeonewa, umesingiziwa, unanyanyaswa.. mwachie
Mwenyezi MUNGU afanye maamuzi.
Haya mzikaji aliyetegemea atamfukua naye ni maiti, tazama
mateso atakayoyapata hadi kufa kwake. Bila shaka atatamani kurudi
gerezani kwa miaka mingine kumi lakini haitawezekana tena.
SOMA MKASA HUU WA KWELI UNAOSISIMUA NA KUTISHA ILA WENYE MAFUNZO YA KUTOSHA KWETU SISI.
Reviewed by crispaseve
on
12:57
Rating:

Post a Comment