VAN PERSIE AIBEBA MAN UTD, YAFUZU ROBO FAINALI KWA KUITANDIKA OLYMPIAKOS 3-0, WAUNGANA NA DORTMUND.
STRAIKA wa kimataifa wa uholanzi, Rob Van Persie ameonyesha
makali yake kwa kuifungia ‘Manchester United’ goli tatu ‘Hat Trik’
katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani ulaya na kuiwezesha kufuzu
hatua ya robo fainali kwa ushindi wa bao 3 -0 dhidi ya
Olympiakos ya ugiriki na kuwasahaulisha wapenzi wa timu hiyo kipigo cha
bao 3 walichokipata kutoka kwa mahasimu wao, klabu ya Liverpool katika
dimba la Old Trafford.
Huko nchini Ujerumani pamoja na Dortmund kufungwa nyumbani
kwenye uwanja wa Signal Iduna Park mabao 2-1 na Zenit St Petersburg ya
nchini Urusi,ilifanikiwa kuingia hatua ya robo fainali ya michuano hiyo
ya ligi ya mabingwa barani ulaya kwa jumla ya mabao 5-3.
mabao ya Zenit hapo jana usiku yalifungwa na mshambuliaji
raia wa Brazil Hulk kwa shuti kali na lingine lilifungwa na Salomon
Rondon wakati lile la Dortmund lilifungwa na kiungo mkongwe Sebastian
Kehl.
Wachezaji wa Borrusia Dortmund wakishangilia bao lao.
VAN PERSIE AIBEBA MAN UTD, YAFUZU ROBO FAINALI KWA KUITANDIKA OLYMPIAKOS 3-0, WAUNGANA NA DORTMUND.
Reviewed by crispaseve
on
13:45
Rating:

Post a Comment