USIKU WA MATUMAINI 2014… HISTORIA KUANDIKWA UPYA
“Historia itaandikwa upya na kwamba Watanzania wakae tayari kuisubiri Agosti 8, mwaka huu, muda si mrefu tutaanza kutaja orodha kamili ya wasanii wakubwa tutakaokuwa nao ambao kwa hakika itakuwa ni sapraizi kwa mashabiki wa burudani Bongo,” alisema Maloto na kuongeza:
“Kama kawaida, Tamasha la Usiku wa Matumaini litafanyika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, ule mpya, mkubwa.”
Tamasha la Usiku wa Matumaini huandaliwa na Kampuni ya Global Publishers, ambapo linachukua nafasi kila mwaka na linawakutanisha watu wengi kutokana na matukio mbalimbali yanayolipamba tamasha hilo.
Miongoni mwa matukio ambayo yalisisimua mwaka jana kwenye tamasha hilo ni pamoja na mechi za mpira wa miguu kati ya wabunge, ndondi za wabunge, mechi za Bongo Fleva na Bongo Movie, bendi mbalimbali kutumbuiza pamoja, mastaa mbalimbali wa muziki wa Gospo kutoka ndani na nje ya Bongo.
USIKU WA MATUMAINI 2014… HISTORIA KUANDIKWA UPYA
Reviewed by crispaseve
on
23:55
Rating:

Post a Comment