Chuo Kikuu Cha Dar es Salaa (UDSM) Yakanusha Kumtunuku Mwanamuziki Mahiri Naseeb Abdul- Diamond Platnumz Shahada ya PHD

Diamond Platnumz
---
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimekanusha ujumbe
uliopo katika mitandao ya kijamii ambao unadai kuwa msanii wa kizazi
kipya Naseeb Abdul maarufu kama Diamond atanukiwa Shahada ya Uzamivu ya
heshima katika mahafali ya 44 yanayotarajiwa kufanyika Novemba 8.
Ujumbe huo ambao ulieleza kuwa Diamond atakabidhiwa shahada
hiyo sawa na aliyekuwa mkuu wa chuo hicho marehemu Balozi Fulgence
Kazaura katikati mahafali yatakayofanyika katikati ukumbi wa Mlimani
City.
Akizungumzia habari
hiyo, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa
Yunus Mgaya alisema hakuna kitu kitu kama hicho – ni uzushi.
Chuo Kikuu Cha Dar es Salaa (UDSM) Yakanusha Kumtunuku Mwanamuziki Mahiri Naseeb Abdul- Diamond Platnumz Shahada ya PHD
Reviewed by crispaseve
on
09:32
Rating:
Reviewed by crispaseve
on
09:32
Rating:

Post a Comment