WAKENYA WAWAFUNIKA WATANZANIA MICHUANO YA TENISI DAR OPEN
Mmoja
wa wadhamini kutoka kampuni ya mawikili ya IMMA ya Dar es Salaam,
Alexander Sarac, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa michuano
ya tenisi ya walemavu ya kimataifa kutoka Tanzania kwa udhamini mkuu wa
kampuni ya magari ya CFAO Motors kupitia brandi ya magari ya Mercedes
Benz. (Picha na Zainul Mzige wa MOblog).
Na Mwandishi wetu
WACHEZA
tenisi kutoka nchini Kenya wamewafunika watanzania katika michuano ya
kimataifa ya kwanza ya tenisi kwa walemavu (Dar Open ). Michuano hiyo
inatarajiwa kuhitimishwa kesho katika viwanja vya Gymkhana, majira ya
saa 10 ambapo washindi watapewa tuzo zao.
Kwa
mujibu wa matokeo ya hadi mchana wakati mwandishi wa habari hizi
anaondoka viwanjani hapo, mechi saba zilienda kwa wakenya kwa nafasi ya
wanaume na wanawake na mbili ndio walishinda Watanzania.
Michuano
hiyo ambayo inadhaminiwa na kampuni ya magari ya CFAO, Mercedes-Benz
na kampuni ya mawakili ya Dar es salaam ya IMMMA imelenga pia kuandaa
wachezaji kwa ajili ya mechi za kufuzu michezo ya dunia zinazotarajiwa
kupigwa nchini Kenya Februari mwakani.
Mshiriki
wa michuano ya tenisi ya walemavu ya kimataifa kutoka Tanzania, Rehema
Selemani akirusha mpira wakati akichuana na mshiriki kutoka Mombasa,
Phoebe Masika (hayupo pichani).
Kwa
mujibu wa msemaji wa wadhamini wa michuano hiyo Alexander Sarac,
michuano hiyo yenye washiriki wanaume 17 na wanawake watano walioitwa
kutoka Tanzania na Kenya, imelenga kuwezesha walemavu kuendeleza vipaji
vyao vya kucheza tenisi.
Pamoja
na kuwa na ushindi dhaifu wa watanzania kocha wa timu ya Tanzania
amesema bado ana bunduki zake mbili na ana hakika kesho vikombe vitabaki
Tanzania. Fungua dimba ya michuano hiyo ilianzishwa na watanzania
Novatus Temba na Moses Sebastian ambapo Temba alimchapa Sebastian kwa
seti 2-0; mkenya Itaken Timoi alimvuruga Bernad Antony kwa seti 2-0 huku
Mkenya mwingine Peter Mnuve akimtoa Mtanzania Albert John kwa seti
2-0.
Katika
michezo mingine Rajab Abdallah kutoka Kenya alimtoa Adil Hashim kwa
seti 2-0 huku Yohana mwila wa Tanzania akimpa taabu Kenya ambaye
alimuondoa kwa seti 2-1. Muingereza anayeishi nchini Ian Artetiel
alimtoa Mtanzania Voster Peter kwa seti 2-1.
WAKENYA WAWAFUNIKA WATANZANIA MICHUANO YA TENISI DAR OPEN
Reviewed by crispaseve
on
07:55
Rating:

Post a Comment