Header AD

Maonyesho ya Harusi Trade Fair 2015 kufanyika Machi 13-14 ndani ya Danken House

Ofisa Mtendaji Masoko wa EATV, Brendansia Kileo (kulia) akifafanua jambo mbele ya wandishi (hawapo pichani), kushoto kwake ni Digital &Branding Manager wa 361 degree, Hurbert Kissas na kulia ni Meneja wa chapa wa vinywaji vikali wa Serengeti Breweries Limited, Shomari Shija.
Maonyesho ya siku mbili ya Harusi Tanzania maarufu kama ‘Harusi Trade Fair 2015’, yanayotarajiwa kufanyika Machi 13-14 mwaka huu katika ukumbi wa Danken House, uliopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.
 
Wakiongea na wandishi wa habari  mapema jana Machi 2, wakati wa kutambulisha wadhaamini wakuu wa mwaka huu ambao ni kampuni ya Bia ya Serengeti, kupitia kwa vinywaji vya Baileys ‘Cream with Spirit’ na Johnnie Walker ‘Gold Label’, wandaaji wa maonyesho hayo kampuni ya 361 degree, kupitia kwa Meneja biashara na maendeleo,  Hamis Omary alisema tayari maandalizi hayo yamepamba moto huku washiriki zaidi ya 50, wakitarajiwa kushiriki.
 
“mwaka huu ni wa sita kwa maonyesho haya. Hivyo tunajivunia mafanikio mbalimbali. Tunashukuru wadhamini wetu kampuni ya bia ya  Serengeti kwa kujitokeza  kudhamini mwaka huu ni faraja kwetu” alisema Hamis Omary.
Maonyesho ya Harusi Trade Fair 2015 kufanyika Machi 13-14 ndani ya Danken House Maonyesho ya Harusi Trade Fair 2015 kufanyika Machi 13-14 ndani ya Danken House Reviewed by crispaseve on 07:48 Rating: 5

No comments

Post AD