Header AD

Elimu ya uongozi bora yatolewa kwa viongozi wa vikundi vya vijana Kata ya Selela

 Mhamasishaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Ester Riwa katikati akizungumza na Vijana wa Kata ya Selela (hawapo pichani) wakati wa semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana jana katika Kata ya Selela Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha. Kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele na kulia ni Afisa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara hiyo Bi. Amina Sanga
 
 Vijana wa Kata ya Selela wakisikiliza kwa makini mada zilizokua zikitolewa wakati wa semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana jana katika Kata ya Selela Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha.
 Afisa Maendeleo ya Vijana kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Bi. Mesha Singoyo akifafanua jambo kwenye semina ya vijana wa Kata ya Selela kuhusu Ujasiriamali, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyofanyika jana katika Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha
 Afisa Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga (kulia) akizungumza na wanakikundi cha Naisho wanaomiliki mradi wa kunenepesha ng’ombe na kuziuza wakati wa kutembelea miradi ya vijana wa Kata ya Selela Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha. Wapili kushoto ni mhamasishaji kutoka Wizara hiyo Bibi. Ester Riwa na wanne kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele.
 Baadhi ya ng’ombe zinazomilikiwa na vijana wa Naisho Group zikiwa machungani katika kata ya Selela Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha.
 Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele (wapili kulia) akifafanua jambo walipotembelea mradi wa kikundi cha Songambele kinachojishughulisha na kilimo katika Kata ya Selela Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha. Kulia ni mhamasishaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Ester Riwa.
Moja ya shamba la mahindi linalomilikiwa na kikundi cha Songambele katika kata ya Selela Halmashauri ya Wilaya ya Mondili Mkoani Arusha. Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo, Monduli
Elimu ya uongozi bora yatolewa kwa viongozi wa vikundi vya vijana Kata ya Selela Elimu ya uongozi bora yatolewa kwa viongozi wa vikundi vya vijana Kata ya Selela Reviewed by crispaseve on 02:41 Rating: 5

No comments

Post AD