Kumbukumbu ya Amina Ngaluma J’mosi Dar
.jpg)
KISOMO
cha kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo cha aliyekuwa mwimbaji mahiri
nchini, marehemu Amina Ngaluma ‘Japanese’ kinatarajiwa kufanyika
Jumamosi wiki hii Kitunda, Machimbo Dar es Salaam.
Akizungumza
na gazeti hili, baba mzazi wa marehemu, Kassim Ngaluma, alisema kisomo
hicho kitafanyika nyumbani kwa wazazi wake marehemu na kuwaomba ndugu,
jamaa na marafiki mbalimbali wa marehemu wakati wa uhai wake wahudhurie.
“Tunaomba
wote tulioshiriki kwa namna mbalimbali wakati wa msiba wa marehemu
mwanangu, tushirikiane pia katika kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo
chake,” alisema Mzee Ngaluma na kuongeza kuwa kisomo hicho kitafanyika
saa saba mchana baada ya swala ya adhuhuri.
Aliwaomba
waliokuwa wanamuziki wenzake na marehemu, mashabiki wake, pamoja na
wadau wengine wa muziki na marafiki wote, washirikiane katika tukio
hilo.
Ngaluma
aliyepata kung’ara na bendi mbalimbali nchini, alifariki dunia Mei 15
mwaka jana kwa shinikizo la damu akiwa Thailand alikokuwa akifanya
shughuli za muziki katika bendi ya Jambo Survivor na kuzikwa Mei 24
mwaka huo, Dar es Salaam.
Wakati
wa uhai wake alitamba na bendi mbalimbali zikiwemo African Revolution
‘Tamtam’, Double M Sound ‘Mshikemshike’ na TOT Plus zote za Dar es
Salaam.Pia alipigia makundi ya Arusha Sangoma, Sayari Band na Less
Mwenge yote ya Arusha na Mangelepa na Sky Sound za Kenya.
Baadhi
ya nyimbo alizotunga wakati wa uhai wake ni Manyanyaso Kazini na
Mapendo alizotunga akiwa Tamtam, wakati Double M Sound alitunga nyimbo
za Wajane na Ukewenza.Pia alitoa albamu yake binafsi iitwayo Jitulize.
Baadhi
ya nyimbo alizopata kuimba na kumpatia umaarufu mkubwa ni Mgumba,
Maisha Kitendawili, Ndugu Lawama, Zawadi ya Watanzania, Ugumu wa Maisha
na Call Box zote zikitungwa na Muumin Mwinjuma ‘Kocha wa Dunia’.
Kumbukumbu ya Amina Ngaluma J’mosi Dar
Reviewed by crispaseve
on
10:52
Rating:
Reviewed by crispaseve
on
10:52
Rating:

Post a Comment