SPORTS XTRA NDONDO CUP YAZINDULIWA RASMI, ABAJALO, FC KAUZU MUZIKI WAO..OGOPA SANA!
Msimu
wa pili wa mashindano ya Sports Xtra Ndondo Cup chini ya udhamini wa
Dr. Mwaka, Daktari bingwa wa masuala ya Afya ya uzazi na Tiba asilia
kutoka kituo cha Foreplan Clinic, kilichopo Bungoni, Ilala, Dar es
salaam umezinduliwa rasmi katika uwanja wa Bandari, Tandika, jijini Dar
es salaam.
Mechi
ya ufunguzi yenye mvuto wa aina yake imepigwa jana ikiwakutanisha
mabingwa watetezi, Abajalo FC ya Sinza Dar es salaam dhidi ya timu
iliyojizolea Umaarufu ya wauza mitumba wa Tandika, FC Kauzu na hadi
dakika 90 zinamalizika wanaume hao wa ‘Shoka’ walitoka suluhu (0-0).
Mashabiki
zaidi ya Elfu tano walihudhuria mechi hiyo iliyojaa vitimbwi, mbembwe
za kila aina na nimekuwekea baadhi ya picha zikionesha shamrashamra za
mashabiki wa Sports Xtra Ndondo Cup Chini ya udhamini wa Dr. Mwaka.
SPORTS XTRA NDONDO CUP YAZINDULIWA RASMI, ABAJALO, FC KAUZU MUZIKI WAO..OGOPA SANA!
Reviewed by crispaseve
on
05:54
Rating:

Post a Comment