Header AD

IJUE LISTI YA WALIOSHINDA UVCCM TAIFA!!


HONGERENI SANA!!! UVCCM HOYEEEE

MWENYEKITI UVCCM TAIFA NI Mhe. JUMA SADIFA - 2012-2017
MAKAMU MWENYEKITI UVCCM TAIFA NI Mhe.MBONI MHITA

WAJUMBE NEC
1. Jerry Silaa [Mayor wa Ilala]
2. Deo Ndejembi
3. Anthony Mavunde Sosa [Wakili Msomi]
4. Jonas Nkya [Wakili Msomi]
5. Petro Magoti [mlemavu wa viungo]
6. Fatma Jumbe [mlemavu wa Ngozi]



 By Maisha Times.
Habari zaidi zinasema kwamba Uchaguzi wa UVCCM uliokuwa ukiendelea huko Dodoma ulitawala vimbwanga kwa watu kutoa Rushwa kana kwamba ni agizo la chama!! Vijana wanaosemekana kwamba wanabebwa na baadhi ya vigogo wa muda mrefu katika chama [CCM] wamemwaga Rushwa pasipo kuiogopa Takukuru!!!
Katika uhalisia Chaguzi zote za ndani ya Chama Cha Mapinduzi [CCM] zimegubikwa na rushwa ya kutisha! Sumaye alitamka hivyo siku kadhaa zilizopita. Na sasa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, amethibitisha bila shaka yoyote kuwa rushwa ndani ya chaguzi kwenye jumuiya zote za CCM, ikiwemo UWT na UVCCM, ni ya kutisha na inaelekea kukizika chama hicho kikongwe hapa nchini. 
Mimi kama mwanahabari mchanga ninayechipukia nina swali dogo tu la kumuuliza Jk: Kama hilo analijua na zaidi anajua vyema kwamba chaguzi zote za ndani ya CCM, huwa vijana wa Hoseah [Takukuru] huwa wanajaa, wakijidai kwamba wanadhibiti rushwa je kama hiyo TAKUKURU inashindwa kufanya kazi inayotakiwa kuifanya na badala yake rais anabaki kulalamika badala ya kuchukua hatua ya kuivunja je hapo sasa mh rais na Mwenyekiti wa CCM taifa anataka sisi kama Wananchi tumweleweje? Tunajua wazi kwamba Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupamaba na Rushwa Tanzania [TAKUKURU] Dk Edward Hosea ameteuliwa na rais kusimamia chombo hicho muhimu cha kudhiti na kuzuia vitendo vya rushwa nchini sasa kama mhusika ameshindwa kazi basi rais anapaswa kumfukuza kazi na wala si kubaki kuwalalamika wananchi kama tulivyoweza kuthibitisha katika siku chache zilizopita, kinyume na hapo basi tuseme kwamba kama safari hii mh rais asipomfukuza kazi Dk Hosea na kubaki kulalamika tutajua wazi kwamba kinachoendelea ni maigizo ya kawaida ya Chama Cha Mapinduzi.
Reviewed by crispaseve on 04:54 Rating: 5

No comments

Post AD