IJUE LISTI YA WALIOSHINDA UVCCM TAIFA!!
HONGERENI SANA!!! UVCCM HOYEEEE
MWENYEKITI UVCCM TAIFA NI Mhe. JUMA SADIFA - 2012-2017
MAKAMU MWENYEKITI UVCCM TAIFA NI Mhe.MBONI MHITA
WAJUMBE NEC
1. Jerry Silaa [Mayor wa Ilala]
2. Deo Ndejembi
3. Anthony Mavunde Sosa [Wakili Msomi]
4. Jonas Nkya [Wakili Msomi]
5. Petro Magoti [mlemavu wa viungo]
6. Fatma Jumbe [mlemavu wa Ngozi]
By Maisha Times.
Habari zaidi zinasema kwamba Uchaguzi wa UVCCM uliokuwa ukiendelea huko
Dodoma ulitawala vimbwanga kwa watu kutoa Rushwa kana kwamba ni agizo la
chama!! Vijana wanaosemekana kwamba wanabebwa na baadhi ya vigogo wa
muda mrefu katika chama [CCM] wamemwaga Rushwa pasipo kuiogopa
Takukuru!!!
Katika uhalisia Chaguzi zote za ndani ya Chama Cha Mapinduzi [CCM]
zimegubikwa na rushwa ya kutisha! Sumaye
alitamka hivyo siku kadhaa zilizopita. Na sasa Mwenyekiti wa CCM na Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya
Kikwete, amethibitisha bila shaka yoyote kuwa rushwa ndani ya chaguzi
kwenye jumuiya zote za CCM, ikiwemo UWT na UVCCM, ni ya kutisha na
inaelekea kukizika chama hicho kikongwe hapa nchini.
Mimi kama mwanahabari mchanga ninayechipukia nina swali dogo tu
la kumuuliza Jk: Kama hilo analijua na zaidi anajua vyema kwamba chaguzi
zote za ndani
ya CCM, huwa vijana wa Hoseah [Takukuru] huwa wanajaa, wakijidai kwamba
wanadhibiti
rushwa je kama hiyo TAKUKURU inashindwa kufanya kazi inayotakiwa
kuifanya na badala yake rais anabaki kulalamika badala ya kuchukua hatua
ya kuivunja je hapo sasa mh rais na Mwenyekiti wa CCM taifa anataka
sisi kama Wananchi
tumweleweje? Tunajua wazi kwamba Mkurugenzi wa Taasisi
ya Kuzuia na Kupamaba na Rushwa Tanzania [TAKUKURU] Dk Edward Hosea
ameteuliwa na rais kusimamia chombo hicho muhimu cha kudhiti na kuzuia
vitendo vya rushwa nchini sasa kama mhusika ameshindwa kazi basi rais
anapaswa kumfukuza kazi na wala si kubaki kuwalalamika wananchi kama
tulivyoweza kuthibitisha katika siku chache zilizopita, kinyume na hapo
basi tuseme kwamba kama safari hii mh rais asipomfukuza kazi Dk Hosea na
kubaki kulalamika tutajua wazi kwamba kinachoendelea ni maigizo ya
kawaida ya Chama Cha Mapinduzi.
Reviewed by crispaseve
on
04:54
Rating:
Post a Comment