Header AD

YANGA B WAITILIA UBANI YANGA A, WAYACHAPA KIDUDE MAKINDA YA MGAMBO


Timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Yanga, imeifunga Mgambo JKT ya vijana pia, bao 1-0 katika mchezo wa utangulizi, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kabla ya kuanza kwa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baina ya kaka zao, Yanga A dhidi ya Mgambo JKT ya Handeni, Tanga. Bao hilo pekee lilitiwa kimiani na Clever Charles dakika ya 65.
Zuberi Amiri wa Yanga B, akichuana na Charles Domayo wa JKT Mgambo

Joseph Banda wa Yanga B (25) akipasua ukuta wa Mgambo

Meshack Ramadhani wa Yanga kushoto akigombea mpira na beki wa Mgambo

Banda akifumua shuti mbele ya mabeki wa Mgambo, mmoja akijaribu kuzuia

Notikel Masasi wa Yanga B akiwa chini ya ulinzi wa mabeki wa Mgambo

Kocha Ernie Brandts akifuatilia vipaji Yanga B ikicheza na Mgambo

Notikel Masasi wa Yanga B, akichuana na mchezaji wa Mgambo

Clever Charles, mfungaji wa bao la Yanga B leo, akiwa benchi baada ya kupumzishwa. Kulia kwake ni Said Manduta

Reviewed by crispaseve on 09:36 Rating: 5

No comments

Post AD