TASWIRA YA UZINDUZI WA FILAMU YA FOOLISH AGE YA ELIZABETH MICHAEL A.K.A LULU NDANI YA MLIMANI CITY.
Elizabeth Michael (Lulu) akiwasili kwenye ukumbi wa
Mlimani City jijini Dar es salaam tayari kwa uzinduzi wa filamu yake
inayokwenda kwa jina la Foolish Age iliyotengenezwa na Kampuni ya Proin
Promotion chini ya Mwenyekiti wake Jonson Lukaza ambaye ameweza
kujitolea kwa hali na mali mpaka kufanikisha utengenezaji wa filamu hii
na uzinduzi kwa ujumla, Uzinduzi huo unafanyika usiku huu.
Lulu akilakiwa kwa mbwembwe na vijana walioandaliwa kwa kazi hiyo.
Mwenyekiti wa kampuni ya Proin Promotion Bw. Jonson
Lukaza katikati akizungumza na baadhi ya waigizaji wa filamu Rich Rich
na mwenzake .
baadhi ya wageni wake waliohudhuria katika uzinduzi wa filamu hiyo .
Muigizaji wa filamu Jacob Steven akizungumza na wageni wa kampuni ya Proin Promotion katika uzinduzi huo .
Muigizaji Vicent Kigosi Ray akiwasili katika uzinduzi huo unaofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City.
Msanii wa muziki Lady Jay Dee aka Komando aka Anaconda
akituzwa wakati akitoa burudani safi sana katika Uzinduzi wa Lulu ndani
ya Ukumbi wa Mlimani city uzinduzi unaoendelea Muda huu.
Elizaberth Michael (Lulu) akizungumza na wageni
waalikwa katika uzinduzi wa filamu ya Foolish Age iliyotengenezwa na
Kampuni ya Proin Promotion chini ya Mwenyekiti wake Jonson Lukaza
ambaye ameweza kujitolea kwa hali na mali mpaka kufanikisha utengenezaji
wa filamu hii na uzinduzi kwa ujumla, Uzinduzi huo unafanyika usiku
huu.
Waigizaji wa filamu na wageni mbalimbali wakifuatilia filamu ya Lulu.
Tapeli Dude akifanya mambo yake wakati wa uzinduzi huo.
Mwanamuziki Barnaba Classic akiimba kwenye uzinduzi huo.
Wageni waalikwa mbalimbali wakiwa katika uzinduzi huo.
Elizabeth Michael (Lulu) akiwasili kwenye ukumbi wa
Mlimani City jijini Dar es salaam tayari kwa uzinduzi wa filamu yake
inayokwenda kwa jina la Foolish Age.
Mwenyekiti wa Kampuni ya Proin Promotion akizungumza na wageni waalikwa katika hafla ya uzinduzi wa filamu ya Foolish Ege.
Reviewed by crispaseve
on
02:06
Rating:
Post a Comment