KANYE WEST AIBWAGA NIKE NA KUSAINI MKATABA NA KAMPUNI YA ADIDAS
Hatimaye mwanamuziki Kanye West ameamua kutema dili na
kampuni ya Nike aliyokuwa ameingia nayo mkataba hapo awali iliyokuwa
kimtengenezea rapa za Nike Air Yeezy Era, Rapa huyo ambaye kwa sasa
amesaini dili nono na kampuni ya ADIDAS aliweza kufunguka mengi kupitia
mahojiano aliyofanyiwa na kituo cha radio cha Hot 97 pamoja na BBC.
Katika mahojiano hayo Kanye west alinukuliwa akisema kwamba
mkurugenzi mkuu wa NIKE Mark Parker alimuhaidi kumtengenezea matoleo
mawili kila mwaka sambamba na nguo ambazo angekuwa akizibuni yeye
mwenyewe lakini akasema anachoangalia ni maslahi na sio hivyo vitu huku
akitoa mfano wa mcheza kikapu kama Michael Jordan kulipwa Dola Milioni
100 kila mwaka ikiwa ni takribani 5% ya shea yake na NIKE, taarifa
zinasema kwamba kulingana na maslahi anayohitaji Kanye
kutoka Nike isingeweza kumtimizia kutokana yeye sio mwanamichezo
professional ndipo Rapa huyo akaamua kumwaga wino wake na kampuni ya
ADIDAS huku chanzo kikubwa kikiwa ni suala zima la
maslahi, Kampuni hizi mbili ya Nike pamoja na Adidas ni kampuni zilizopo
katika ushindani mkubwa huku zikitengeza bidhaa mbalimbali kama viatu,
soksi, tshirt, vest, mipira na vifaa mbalimbali vya michezo.
Reviewed by crispaseve
on
13:07
Rating:
Post a Comment