PICHA ZA SHOW NZIMA YA MAPACHA PSQUARE WALIVYOKONGA NYOYO ZA WABONGO USIKU WA KUAMKIA LEO VIWANJA VYA LEADERS CLUB DAR ES SALAAM.
Jumamosi hii, P-Square wamefanikiwa kudhihirisha
kwanini wao ni namba moja Afrika na wanastahili kuwa kundi la muziki
linalolipwa fedha nyingi zaidi, baada ya kuzikonga nyoyo za mashabiki wa
Dar es Salaam kwa show kali, yenye nguvu, ya kutikisa na ndefu kwenye
viwanja vya Leaders Club.
Paul akipanda stejini
P-Square ambao walisindikizwa na bendi yenye watu wanne tu
(mpiga drums, mpiga kinanda, mpiga gitaa la bass na gitaa la solo),
walitoa mfano wa namna live show inavyotakiwa kufanywa. Wakitaniana mara
kwa mara jukwaani na kuendesha mashindano ya wao kwa wao, Peter na Paul
Okoye walipiga show ya takriban masaa matatu, kwa kasi, nguvu na uwezo
ule ule, kuanzia mwanzo hadi mwisho.
Peter akiimba wimbo kwa hisia kali
Ilikuwa ni mpaka usikilize kwa makini kutofautisha kile
bendi hiyo na wao walivyokuwa wakiimba na wimbo uliorekodiwa, kwakuwa
bendi hiyo kali inayojua muziki ilipiga nyimbo zao kwa ustadi mkubwa.
Paul akiimba kwa hisia pia
P-Square waliimba karibu nyimbo zote zao zilizotamba na
kuufanya umati mkubwa uliojitokeza Leaders upige kelele muda wote na
kuimba nao nyimbo hizo. Kwa maneno yao wenyewe, P-Square wamesema show
ya Dar ambayo iliandaliwa na East Africa Radio na kudhaminiwa na
Vodacom, ilikuwa ya kuvutia kuliko zote walizowahi kufanya Afrika
Mashariki.
Pamoja na nyimbo zao, pia waliimba nyimbo za wasanii wengine kama Usher, 2face, Radio n Weasel na wengine.
Mpiga gitaa wa P-Square
Awali kabla ya P-Square, Ben Pol, Lady Jaydee na Joh Makini
pamoja na Weusi walitangulia kwa show zilizoshangiliwa kwa kiasi
kikubwa pia. Kwa ufupim show ya P-Square imefanikiwa sana.
Miongoni mwa matukio yaliyotia fora ni pamoja na mrembo
huyo chini kupandishwa jukwaani na kupewa cheo (kwa utani) cha mke wa
pili wa Peter aliyefunga ndoa juzi jijini Lagos.
Mrembo aliyepandishwa jukwaani na P-Square kutambulishwa kama Onyinye wa Tanzania
Peter amkibusu mrembo huyo
Onyinye akivishwa saa na Peter
Paul akivuta hisia
Paul akiwajibika jukwaani
Paul Okoye
Peter akimsikiliza kaka yake Paul
Peter akitafakari kitu
Peter akiuangalia kwa tabasamu umati mkubwa uliojitokeza Leaders Club
Peter akiwa haamini umati mkubwa uliojitokeza Leaders
Peter mara baada ya kubaki kifua wazi
Peter mara baadaya kuvua nguo ya juu
Profesa Jay
Waimbaji wa Machozi Band
Weusi wakiwa stejini
Ben Pol akisindikizwa na bendi ya Machozi akitoa burudani
Ben Pol akitumbuiza
Joh Makini
Lady akiwa ndani ya mavazi kama ya askari wa kike
Lady Jaydee pamoja na Machozi Band akitumbuiza
MC wa pili wa shughuli, T-bWAY
MC wa shughuli, Dulla akisherehesha
Mpiga gitaa wa P-Square
Nikki wa Pili baada ya kupanda kumpa shavu kaka yake Joh Makini
Nikki wa Pili
Beautiful Onyinye wa Tanzania aliyechaguliwa na P-Square
Esi, Jokate na Martin Kadinda
Faiza akifurahia burudani.
Faiza wa EATV akichukua picha
Jokate Mwegelo
Mashabiki wa burudani wakifurahia bia wakati burudani ikiendelea
Mrembo wa kizungu akiangalia shughuli ya P-Square.
Mrembo wa mwenye nguo nyeupe alitia fora baada ya kuitwa
jukwaani na Peter na kupewa heshima ya kuwa Beautiful Onyinye wa
Tanzania.
Mzungu huyu aliyejichora tatto mwili mzima aliamua kusogea karibu pia kuwashuhudia P-Square
Rihanna wa Bongo akijimwaya na burudani ya mapacha hao wa Nigeria.
Rihanna wa Bongo.
Shabiki wa P-Square akiwa ameshika bango lenye ujumbe maalum kwa mapacha hao
Show ilihudhuriwa na watu wa mataifa mbalimbali
Wapenzi wakidokezana jambo
Zari aka The Boss Lady wa Uganda akichukua picha za P-Square.
Zari aliamua kusafiri kutoka Kampala, Uganda kuja kuwashuhudia P-Square.
PICHA ZA SHOW NZIMA YA MAPACHA PSQUARE WALIVYOKONGA NYOYO ZA WABONGO USIKU WA KUAMKIA LEO VIWANJA VYA LEADERS CLUB DAR ES SALAAM.
Reviewed by crispaseve
on
13:18
Rating:
Post a Comment