KING CLASS MAWE ASAINI MKATABA WA KUPAMBANA NA COSMAS CHEKA
BONDIA
bora wa mwaka 2013,2014 katika uzito wa KG 63 Ibrahimu Class 'King
Class Mawe' (pichani) amesaini mkataba wa kupambana na Cosmas Cheka
Februari 8 mwaka huu katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam.
Mara
baada ya kusaini mkataba huo wa kucheza raundi 10 za ubingwa wa Taifa Kg
60 amesema atafanya mazoezi ya kutosha kuhakikisha ana msambaratisha
mpinzani wake raundi za awali kwa kuwa alikuwa anachonga sana juu yake.
Mpambano
huo unaodhaminiwa na Promota Maarufu nchini Jay Msangi utakuwa na
msisimko wa aina yake kutokana na mabondia hawo kuwa gumzo katika
ulimwengu wa masumbwi ndani na nje ya nchi.
King
Class aliongeza kwa kusema;"Nipo fiti, nimejiandaa na ninasubiri tu
kuvishwa ubingwa huo wa Taifa kwani Cheka hana ujanja kwangu mbinu zake
zote nimesha zikamata".
King
Class Mawe ananolewa na jopo la makocha wanao ongozwa na Habibu
Kinyogoli 'Masta' Rajabu Mhamila 'Super D' na Kondo Nasoro.
Bondio
huyo amewashukuru wadau wa mchezo wa ngumi kwa kumuwezesha kuchaguliwa
kuwa bondia bora wa mwaka katika uzito wake na kuwapita mabondia wengine
wanne na yeye kuibuka kidedea katika kin'yan'gan'yiro hicho.
KING CLASS MAWE ASAINI MKATABA WA KUPAMBANA NA COSMAS CHEKA
Reviewed by crispaseve
on
05:31
Rating:
Post a Comment