Miaka 10 ya onyesho la ‘Lady in red’ Februari 14, Wabunifu mbalimbali kupamba
Na Mwandishi Wetu
WABUNIFU
mbali mbali kupamba miaka 10 ya onyesho la mavazi lijulikanalo kama
‘Lady in Red Super brand, 10th Anniversary’ linalotarajiwa kufanyika
Februari 14, ambapo pia litatumbuizwa na burudani kutoka kwa Babloom
Trio bendi na Wanne Star, kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Kwa
mujibu wa Mkurugenzi wa Fabak Fashions inayoandaa onyesho hilo, Asia
Idarous Khamsin, alisema tayari maandalizi ya onyesho hilo
yameshakamilika na tayari wabunifu mbalimbali wameanza mchakato wa
kuandaa mavazi yao watakayoonyesha siku hiyo.
Asia
Idarous alipongeza wadau mbali mbali kwa kuliunga mkono onyesho hilo la
‘Lady in red’ hadi kufikisha miaka 10, tokea kuanzishwa kwake, na
kutamba kuwa la kipekee kwa mwaka huu. “Februari 14, mwaka huu ndiyo
siku pekee kwa wadau wa mitindo na urembo ambapo watashuhudia wabunifu
mbalimbali siku hiyo wakipamba jukwaa, wakiwemo wakongwe na wale
wanaochipukia” alisema Asia Idarous.
Na
kuongeza kuwa, kwa mwaka huu wametoa fursa kwa wabunifu wanaochipukia
kuonyesha mitindo yao sambamba na wakongwe ili kuleta changamoto kwen ye
tasnia hiyo ya ubunifu na mitindo hapa nchini.
Aidha,
katika onyesho hilo ambalo litafanyika siku hiyo ya Februari 14, ambayo
pia itakuwa ni siku ya Wapendanao ‘Valentine’s Day’ , kiingilio
kitakuwa sh 30,000 kwa viti vya kawaida huku viti maalum ikiwa sh
50,000, ambapo pia kutakuwa na burudani kutoka bendi ya Babloom Trio na
Mwanamuziki mahiri wa nyimbo na ngoma za asili, Wanne Star.
Asia
Idarous aliyashukuru makampuni mbalimbali ambayo yamejitokeza kudhamini
onyesho hilo wakiwemo kampuni ya nywele ya Darling-‘Quality hair
additions’, na Zanzi ‘Cream liqueur’ ambao ni wadhamini wakuu mwaka
huu. Wengine ni CXC, Times fm, Clouds media, Vijimambo blog, michuzi
media group, channel ten, Elite Computer, Eventlites, One
touch-solution, Raysa Style,Paka Wear, Dj Bula, Magic fm, DTV, Jambo
Leo, I View Vayle Spring, Voice of American na mengine mengi.
Miaka 10 ya onyesho la ‘Lady in red’ Februari 14, Wabunifu mbalimbali kupamba
Reviewed by crispaseve
on
21:01
Rating:
Post a Comment