Waziri Muhongo apata ugeni kutoka nchini Ufaransa
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akiwa pamoja na Balozi
wa Ufaransa nchini Tanzania, Marcel Escure (kulia kwa Waziri) pamoja na
Waziri Mstaafu wa Viwanda na Nishati wa Ufaransa Bw. Eric Besson (kulia
kwa Balozi), pamoja na watendaji kutoka Ubalozi wa Ufaransa na Wizara
ya Nishati na Madini, wakati walipomtembelea wizarani ili kufahamu fursa
za uwekezaji katika sekta hizo.
Waziri
wa Nishati na Madini , Profesa Sospeter Muhongo (wa kwanza kulia) ,
Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Marcel Escure (kulia kwa Waziri),
Waziri mstaafu wa Viwanda na Nishati kutoka nchini Ufaransa Bw. Eric
Besson (kulia kwa Balozi), pamoja na mtendaji kutoka Ubalozi wa
Ufaransa nchini, wakifurahia jambo mara baada ya kumaliza mazungumzo
yaliyolenga katika kuendeleza sekta za Nishati na Madini nchini.
Na Teresia Mhagama
Balozi
wa Ufaransa nchini Bw. Marcel Escure akiongozana na Waziri mstaafu wa
Viwanda na Nishati kutoka nchini Ufaransa, Bw. Erick Besson
wamemtembelea wizarani Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter
Muhongo ili kufahamu fursa za uwekezaji katika sekta za Nishati na
Madini. Waziri huyo mstaafu wa Ufaransa, Bw.Erick Besson alikuwa akiiwakilisha kampuni ya GDF Suez ya Ufaransa. Katika suala la usimamizi wa bomba la gesi asilia, Profesa Muhongo alimweleza Bw. Besson kuwa Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) litahitaji kupata uzoefu na pengine mbia liyebobea katika usimamizi wa bomba hilo atakayeshirikiana na
TPDC katika usimamizi wa bomba la gesi nchini. Kuhusu umeme, Waziri Muhongo alimweleza Waziri mstaafu huyo wa Ufaransa kwamba serikali inajikita katika miradi ya usambazaji umeme kwa utaratibu wa ubia au mikopo ya bei nafuu na ina mpango wa kujenga njia ya umeme ya msongo wa 400kv kuelekea ziwa Tanganyika hivyo aliikaribisha kampuni ya GDF Suez kuwekeza katika miradi hiyo ya usambazaji umeme.Aidha Profesa Muhongo alimweleza Bw. Besson kuwa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) linatafuta mbia watakayeshirikiana naye katika kuendesha mtambo wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe, Kiwira mkoani Mbeya hivyo kama wana nia ya kuwekeza katika eneo hilo pia wanakaribishwa kuingia katika ushindani wa kupata nafasi hiyo.
Naye
Waziri mstaafu wa Viwanda na Nishati kutoka nchini Ufaransa, Bw. Besson
alimshukuru Profesa Muhongo kwa taarifa nzuri kuhusu fursa za uwekezaji
nchini na ameahidi kupata taarifa zaidi za uwekezaji katika mashirika ya
TPDC, STAMICO na TANESCO ili kuona jinsi kampuni ya Suez
itakavyoshirikiana na mashirika hayo katika kuendeleza sekta za Nishati
na Madini.
Waziri Muhongo apata ugeni kutoka nchini Ufaransa
Reviewed by crispaseve
on
05:29
Rating:
Post a Comment