PICHA : WASANII WA MUZIKI TANZANIA WAFANYA VIDEO YA WIMBO WA KUDUMISHA MUUNGANO
Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya
muungano, Wasanii wa fani ya muziki Tanzania wameungana kwa pamoja na
kufanya video ya wimbo wenye dhima ya kudumisha umoja na mshikamano wa
muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar ambao ulitiwa saini na waasisi
wa Taifa letu, Mzee Julius Kambarage Nyerere na Mzee Aman Abeid Karume.
Kama ilivyo miaka ya muungano na ndivyo hivyo idadi ya
wasanii walioshirikiana kwenye wimbo huku kila mmoja akiwa ametupia vazi
la Taifa,. Wimbo huo umejumuisha wasanii wa Bongo Fleva, Taarabu,
Dansi, Gospel na Raga.
PICHA : WASANII WA MUZIKI TANZANIA WAFANYA VIDEO YA WIMBO WA KUDUMISHA MUUNGANO
Reviewed by crispaseve
on
00:19
Rating:
Post a Comment