TASAF YATOA MAFUNZO KWA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI HUKO UNGUJA
Mkurugenzi
Mtendaji wa TASAF , Bwana Ladislaus Mwamanga akiwatambulisha baadhi ya
wageni walioshiriki katika kikao cha kujifunza kutoka kwa walengwa wa
Mpango wa kunusuru kaya Masikini katika shehia ya Mwembemakumbi wilaya
ya Mjini Unguja ambako ujumbe huo umekuweko kwa siku Tatu.
Mkurugenzi
wa Miradi wa TASAF Bwana Amedius Kamagenge akitoa ufafanuzi wa moja ya
masuala yaliyojitokeza katika kikao cha pamoja kati ya walengwa wa
Mpango wa Kunusuru kaya Masikini katika shehia ya Mwembemakumbi wilaya
ya Mjini Unguja na wadau wa maendeleo ambao wamefanya ziara ya siku
TATU kisiwani Unguja.
Baadhi
ya wajumbe kutoka nchi wafadhili waliohudhuria kikao cha walengwa wa
Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika shehia ya Mwembemakumbi wilaya
ya Mjini Unguja wakisikiliza maoni kutoka kwa walengwa wa mpango huo
(hawapo pichani) Nyuma ni Meneja wa Fedha wa TASAF Bwana Nyamuko na
Meneja Ukaguzi wa TASAF Bwana Mziray wakifuatilia mjadala huo.
Mmoja
wa wajumbe wa kamati ya kusimamia Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini
katika Shehia ya Mwembemakumbi ,wilaya ya Mjini Unguja akitoa ufafanuzi
wamaswali yaliyobuliwa na baadhi ya wajumbe kutoka nchi wafadhili wa
mpango huo juu ya namna walengwa wa mpango huo walivyopatikana.
Mkurugenzi
Mtendaji wa TASAF, Bwana Ladislaus Mwamanga (mwenye sharti la draft)
akiwa na wageni kutoka nchini Marekani wakimsikiliza mmoja wa walengwa
wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (hayupo pichani ) katika shehia ya
Mwembemakumbi wakati alipotoa hoja zake juu ya manufaa ya Mpango wa
kunusuru kaya masikini unaoratibiwa na TASAF.
.Mmoja
wa walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya Masikini katika shehia ya
Mwembemakumbi ,wilaya ya Mjini Unguja akitoa mawazo yake juu ya namna
Mpango huo unavyomunufaisha.
Baadhi
ya wajumbe wa nchi wafadhili na viongozi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
TASAF wakielekea kwenye ukumbi ambako wamekutana na walengwa wa Mpango
wa kunusuru kaya masikini katika shehia ya MwembeMakumbi wilaya ya Mjini
Unguja
TASAF YATOA MAFUNZO KWA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI HUKO UNGUJA
Reviewed by crispaseve
on
09:06
Rating:
Post a Comment