Header AD

Miss Universe Tanzania washiriki fashion show Moscow ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanzania

 Betty Boniface
Nelly Kamwelu

Warembo wawili wa waliowahi kushinda taji la Miss Universe, Nelly Kamwelu na Betty Boniface leo (Jumamosi) watapanda jukwaani mjini Moscow, Urusi kushiriki katika maonyesho ya mavazi ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Warembo hao waliondoja nchini juzi na tayari wapo mjini Moscow kwa ajili ya maonyesho hayo ambayo pia yatashirikisha waonyesha mavazi mbali mbali wa Tanzania.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Communications, Maria Sarungi Tsehai alisema jana kuwa warembo wake wamepata heshima hiyo kutokana na ukweli kuwa Miss Universe imefanya kazi kubwa sana ya kuitangaza nchi kimataifa na hasa mwaka jana baada ya mrembo wake, Betty Boniface kufanya vyema mjini Moscow.

Alisema kuwa katika mashindano ya mwaka jana, Betty aliweza kuitangaza nchi vilivyo pamoja na kufanyiwa mahojiano makubwa na vyombo vya habari mbali mbali vya kimataifa na kuitangaza nchi  ikiwa pamoja na sekta ya Utalii.

“Hii ni heshima kubwa ambayo Watanzania inadidi tujivunie, warembo wetu wamepata fursa hiyo kubwa ya kuonyesha maonyesho ya mavazi yaliyoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Urusi, ni nafasi pekee ambayo tumepewa na tunashukuru kuitumia fursa hiyo,” alisema Maria.

Aliongeza kuwa hatua hiyo imewapa hamasa zaidi na kujua umuhimu wa mashindano hayo hasa kwa kufanya vyema katika mashindano mbali mbali. Mwaka 2007, mrembo wa kwanza wa Miss Universe Tanzania, Flaviana Matata alimaliza katika hatua ya tano bora nchini Mexico na kuipaisha nchi. Flaviana kwa sasa anafanya kazi nchini Marekani na ni mmoja wa waonyesha mitindo wa kimataifa.
Miss Universe Tanzania washiriki fashion show Moscow ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanzania Miss Universe Tanzania washiriki fashion show Moscow ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanzania Reviewed by crispaseve on 09:05 Rating: 5

No comments

Post AD