Header AD

CHINA NA TANZANIA ZATILIANA SAINI MKATABA WENYE THAMANI YA DOLA LAKI MOJA ZA KIMAREKANI

PIX 1 (3)Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah akitoa maelezo juu ya kazi mbalimbali zifanywazo na Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania leo wakati wa sherehe fupi ya utiaji saini mkataba wathamani ya dola laki moja za kimarekani kati ya Chama cha Kupunguza matumizi ya silaha na Maridhiano cha China na Ofisi za Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania.
PIX 3 (2)Baadhi ya viongozi toka pande zote mbili wakiwa katika sherehe ya utiaji saini mkataba wa thamani ya dola laki moja za kimarekani kwaajili ya ununuzi wa vifaa vya ofisi za Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania uliofanyika leo ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam.
PIX 5 (2)Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah (kulia) pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha kupunguza Matumizi ya Silaha na Maridhiano cha Jamhuri ya Watu wa China (Chinese Peoples’ Association for Peace and Disarmament) Bi. Chen Huaifan wakitia saini mkataba huo wa thamnai za fedha za kimarekani dola laki moja leo ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam.
PIX 7Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah (kulia) pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha kupunguza Matumizi ya Silaha na Maridhiano cha Jamhuri ya Watu wa China (Chinese Peoples’ Association for Peace and Disarmament) Bi. Chen Huaifan wakitia saini mkataba huo wa thamnai za fedha za kimarekani dola laki moja leo ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam.
PIX 8Katibu wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah (kulia) akimkabidhi zawadi mgeni wake Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha kupunguza Matumizi ya Silaha na Maridhiano cha Jamhuri ya Watu wa China (Chinese Peoples’ Association for Peace and Disarmament) Bi. Chen Huaifan (kushoto) mara baada ya kutia saini mkataba wa makubaliano wenye thamani za fedha za kimarekani dola laki moja leo ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO.
Na. Benedict Liwenga-MAELEZO.
16/05/2014
OFISI ndogo ya Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania leo imetialiana saini na Chama cha kupunguza Matumizi ya Silaha na Maridhiano cha Jamhuri ya Watu wa China (Chinese Peoples’ Association for Peace and Disarmament) wenye thamani ya dola laki moja za kimarekani.
Utaiji saini huo umefanyika leo katika Ofisi ndogo za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukihusisha viongozi wa pande zote mbili akiwemo Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha kupunguza Matumizi ya Silaha na Maridhiano cha Jamhuri ya Watu wa China (Chinese Peoples’ Association for Peace and Disarmament) Bi. Chen Huaifan.
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Thomas Kashililah amesema kuwa mkataba huo wenye thamani ya dola laki moja za kimarekani utasaidia ofisi ya Bunge kuweza kupata vifaa mbalimbali vya ofisi vikiwemo kompyuta, mashine ya kudurufu, vipaza sauti, kamera pamoja na vifaa vya kurekodia.
“Ndugu zetu kutoka China pamoja na hiki Chama chao wamesaini pamoja nasi mkataba wenye thamani ya dola laki moja za kimarekani ambao wametutaka sisi tuamue wenyewe ni vifaa gani tunahitaji kwaajili ya ofisi yetu ya Bunge mjini Dodoma ili wao waweze kutununulia na kutukabidhi”. Alisema Kashililah.
China na Tanzania zimekuwa zikitiliana saini mikataba mbalimbali ya maendeleo ambayo kwa namna moja mikataba hiyo imekuwa ikizinufaisha pande zote mbili kiuchumi na mpaka hivi sasa uhusiano huu umedumu kwa muda miaka hamsin
CHINA NA TANZANIA ZATILIANA SAINI MKATABA WENYE THAMANI YA DOLA LAKI MOJA ZA KIMAREKANI CHINA NA TANZANIA ZATILIANA SAINI MKATABA WENYE THAMANI YA DOLA LAKI MOJA ZA KIMAREKANI Reviewed by crispaseve on 02:34 Rating: 5

No comments

Post AD