Header AD

CHRIS BROWN KUSHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA JELA

Chris BrownUpepo mbaya bado umeendelea kumuandama mwimbaji wa kibao cha Loyal ‘Chris Brown’ ambaye kwa hivi sasa anasotea nyuma ya nondo za jela baada ya upande wa utetezi kubainisha ya kwamba huenda staa huyo akasherekea siku yake ya kuzaliwa akiwa ndani.
Hiyo inakuja kufuatia  jaji Brandlin kutupilia mbali ombi la kupewa dhamana kwa mwanamuziki huyo na kuamuru aendelea kukaa ndani walau kwa wiki moja zaidi mpaka pale tamko  juu ya kesi yake dhidi ya Rihanna litakapokubaliwa baina ya   mwendesha mashitaka na wakili wa nyota huyo ‘Mark Geragos’ kabla ya muda wa kusikilizwa kwa kesi hiyo uliopangwa kufanyika  Mei 09 mwaka huu.
Halikadhalika mwimbaji huyo anaweza akakumbana na adhabu ya kifungo cha miezi sita au zaidi jela endapo  atakutwa na hatia ya kesi iliyokuwa inamkabili mwaka jana ya kumshambulia mtu mmoja nje ya hotel ya W iliyopo jijini Washington Dc marekani.
CHRIS BROWN KUSHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA JELA CHRIS BROWN KUSHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA JELA Reviewed by crispaseve on 01:57 Rating: 5

No comments

Post AD