Header AD

WANENGUAJI WA KHANGA MOKO WAJERUHIWA VIBAYA KWA RISASI

Khanga Moko Laki Si KituWakata nyonga maarufu wa kundi la ‘Khanga Moko Laki Si Pesa’ wamenusurika kupoteza maisha baada ya mtu mmoja kudaiwa kuwashambulia kwa risasi, hali iliyopelekea wasamaria wema kuwakimbiza katika hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya kunusuru maisha yao.

Tukio hilo linaelezwa kutokea wakati wanenguaji hao, Zawia pamoja na mwenzake wakisasambua kwa matarumbeta kwenye harusi kabla ya kufyatuliwa risasi zilizowajeruhi eneo la pajani na mwingine kwenye makalio. Hali za wagonjwa zinatajwa kuimarika  licha ya kulazimika kuendelea kukaa hospitalini hapo kwa matibabu zaidi.
Khanga Moko Laki Si PesaZawia aliyepigwa risasi ya kwenye makalio akiwa kwenye kiti maalum cha wagonjwa katika hospitali ya Mwananyamala
Khanga Moko…..Mnenguaji mwingine wa Khanga Moko aliyepigwwa Risasi ya kwenye Paja


Picha na Geah Habib Wa HekaHeka
WANENGUAJI WA KHANGA MOKO WAJERUHIWA VIBAYA KWA RISASI WANENGUAJI WA KHANGA MOKO WAJERUHIWA VIBAYA KWA RISASI Reviewed by crispaseve on 13:32 Rating: 5

No comments

Post AD