MFUMUKO WA BEI NCHINI UMEPUNGUA - OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU.
Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii na sensa ya Watu na
Makazi Bw. Ephraim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar
es salaam kuhusu kupungua kwa mfumuko wa bei nchini.
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
Ofisi ya
Taifa ya Takwimu imeeleza kuwa mfumuko wa bei nchini kwa mwezi Juni 2014 umepungua ikilinganishwa
na mwezi uliopita kutokana na kupungua kwa bei ya bidhaa na huduma za jamii katika
maeneo mbalimbali.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam
Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii na sensa ya Watu na Makazi Bw. Ephraim Kwesigabo
amesema kuwa mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi Juni, 2014 umepungua na kufikia
asilimia 6.4 kutoka asilimia 6.5.
Amesema kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma mbalimbali kwa mwezi
Juni 2014 imepungua ikilinganishwa na ile iliyokuwepo mwezi Mei kutokana
na hali ya kupungua kwa bei kwenye bidhaa na huduma
MFUMUKO WA BEI NCHINI UMEPUNGUA - OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU.
Reviewed by crispaseve
on
09:27
Rating:

Post a Comment