Header AD

DIAMOND NA DAVIDO HAWANA BIFU ASEMA BABU TALE

Davido X DiamondMeneja wa Diamond, Babu Tale amekanusha kuwepo kwa bifu kati ya Diamond na Davido wakati akizungumza kwenye XXL ya Clouds Fm Ijumaa iliyopita(Dec.09).
Babu Tale amesema wamekuwa na mawasiliano mazuri na menejimenti ya Davido na hata ujumbe aliouandika Davido kwenye ukurasa wake wa Twitter uliomsababishia ashambuliwe na watanzania mapema mwaka jana haukuwa ukimlenga Diamond.
 ”Mimi na management ya Davido tunaongea, hata naweza kukuonyesha meseji za mimi na Kamal ambaye ni meneja wa Davido…na kulingana na….nikunukuu maneno ya Kamal kwangu hata ile meseji ambayo Davido ambayo alipost ya kwanza They Cheated again…. hakuwa anamface Diamond….according to Kamal…akaniambia mbona watanzania wameelewa vibaya”, alisema Tale.
Pia amesema hata tweets ambazo ameandika hitmaker huyo wa Skelewu hivi karibuni hazikuwa zinaamlenga Diamond na kuwataka watanzania wawe wapole.
 ”Sitaki kuamini kama Davido na Diamond wana vita, juzi Davido alikuwa ana-post vitu vyake …sio kwa sababu ya Diamond…watanzania wote washaanza kusema tena oohh Davido anamtukana tena Diamond..hakuna sio hivyo”. 
Unaweza ukatazama Tweets za Davido alizoandika hivi karibuni ambazo zimewafanya mashabiki wa Diamond kudhani huenda kukawa na bifu linaloendelea kati yao.
Davido Tweets

DIAMOND NA DAVIDO HAWANA BIFU ASEMA BABU TALE DIAMOND NA DAVIDO HAWANA BIFU ASEMA BABU TALE Reviewed by crispaseve on 21:55 Rating: 5

No comments

Post AD