Header AD

MSAMA PROMOTIONS LTD YAMWAGA MISAADA KWA VITUO VYA WATOTO YATIMA, YALAANI MAUAJI YA ALBINO YANAYOENDELEA NCHINI

 Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. Alex Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Halima Ramadhan Mlezi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Mwandaliwa kilichopo Tegeta jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, ikiwa ni moja ya misaada inayotolewa katika vituo mbalimbali vya kulelea watoto yatima wakati wa msimu huu wa maadalizi ya Tamasha la Pasaka linalotimiza miaka 15 tangu lianzishwe.

Msama amekabidhi misaada hiyo kwa vituo vitano vya kulelea watoto waishio katika mazingira magumu,makabidhiano ya misaada hiyo ilifanyika kwenye ofisi za kampuni hiyo,Kinondoni jijini Dar.

Msama alisema kuw maandalizi ya tamasha hili yanaendelea vyema mpaka sasa,na kwamba tamasha hilo linatarajiwa kufanyika jijini Dar April 7 2105,ambapo litashirikisha waimbaji mbalimbali wa Kimataifa na wa Nchini,aliongeza kuwa ili kunogesha zaidi tamasha hilo pia kutakuwepo na michezo mbalimbali itakayochezwa ikiwemo na kukabidhi zawadi na vikombe kwa washiriki wa tamasha hilo.

katika hatua nyingine Bwa.Alex Msama amelaani matukio ya mauaji ya Albino hapa nchini,ameiomba Serikali kutilia mkazo katika janga hilo ambalo limekuwa likiibua na kuzua gumzo miongoni mwa jamii,hivyo ameiomba Serikali kuwashughulikia ipasavyo wahusika wote waliofanya na wanaofanya ukatili huo ambao ni kinyume kabisa na maadili ya nchi yetu,na ikibidi kukomesha kabisa matukio hayo ambayo yamekuwa yakilitia aibu Taifa letu.
   Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. Alex Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Honorata Michael  Mlezi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Honorata kilichopo Temeke jijini Dar es salaam.
   Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. Alex Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Rashid Mpinda  Katibu wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Maunga Centre kilichopo Kinondoni Mosco jijini Dar es Sakaam.
   Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. Alex Msama akikabidhi vyakula mbalimbali kwa Soud Said  Mwakilishi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Ijanzo Zanda orphanage Centre cha jijini Dar es salaam


  Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka Bw. Alex Msama akiwa amewabeba baadhi ya watoto wa kituo cha Honorata wakati alipowakabidhi msaada wa vyakula mbalimbali.
MSAMA PROMOTIONS LTD YAMWAGA MISAADA KWA VITUO VYA WATOTO YATIMA, YALAANI MAUAJI YA ALBINO YANAYOENDELEA NCHINI MSAMA PROMOTIONS LTD YAMWAGA MISAADA KWA VITUO VYA WATOTO YATIMA, YALAANI MAUAJI YA ALBINO YANAYOENDELEA NCHINI Reviewed by crispaseve on 08:02 Rating: 5

No comments

Post AD