Header AD

WAZIRI MKUU AAHIDI BWAWA LA KUTUNZIA MAJI NYANZWA

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema anakubaliana na ombi la wakazi wa Nyanzwa na Igunda wilayani Kilolo, mkoani Iringa kuhusu ujenzi wa bwawa la kuhifadhia maji yatakayovunwa msimu wa mvua ili yasaidie kuongeza eneo la mradi wa umwagiliaji.

Ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati akiwahutubia wakazi wa vijiji vya Nyanzwa na Igunda, mara baada ya kukagua mradi wa umwagiliaji wa Nyanzwa ambao ni maarufu kwa kilimo cha vitunguu.

“Huu mradi ni wa siku nyingi. Nimewauliza wataalamu niliokwenda nao wakasema ujenzi wa bwawa ndiyo suluhisho pekee la kuokoa mradi huu na kwamba ni jambo linalowezekana kama fedha zipo.”

Aliutaka uongozi wa mkoa uandae mpango kazi na wauweke kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha ili mradi huo uweze kuombewa fedha kwenye bajeti kuu ya Serikali.  ia aliwataka wakazi wa eneo hilo wakitunze chanzo cha maji kwa kuweka mipaka ili watu wasikivamie na hatimaye kukiharibu.

“Tengeni eneo kwa kuweka mipaka. Mkurugenzi simamia uwekaji wa mipaka kwenye chanzo hiki ili tukilinde kwani uharibifu wa mazingira utakiharibu kabisa,” alisisitiza.

Akiwa katika ukaguzi wa eneo la mradi, Waziri Mkuu alikutana na mkulima mmoja wa vitunguu Bw. Furaha Ngalali (32) ambaye alimweleza kwamba mwaka jana alifanikiwa kulima ekari tatu za vitunguu ambazo zilimpatia kiasi cha milioni 6/- huku kila gunia akiwa ameliuza kwa sh. 70,000/-.

“Gharama kwa kila ekari ni karibu sh. 600,000/- kwa hiyo kwa ekari tatu ni sh. milioni 1.8/-. Tukivuna vitunguu tunaandaa bustani ya mbegu na pia humu tunapanda maharage,” alisema Bw. Ngalali alpoulizwa Waziri Mkuu analima eneo hilo mara ngapi kwa mwaka
WAZIRI MKUU AAHIDI BWAWA LA KUTUNZIA MAJI NYANZWA WAZIRI MKUU AAHIDI BWAWA LA KUTUNZIA MAJI NYANZWA Reviewed by crispaseve on 08:00 Rating: 5

No comments

Post AD