Header AD

Wadau wa Utamaduni washauriwa kutoiga tamaduni za nchi nyingine

UT1 
Kaimu Mkuu wa Idara ya Utamaduni Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Afisa Bw. Habibu Msami akimkaribisha Mgeni rasmi kufunga kikao kazi cha kumi cha sekta ya Utamaduni jana Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mgeni rasmi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw. Raymond Mushi.
UT2 
Mgeni rasmi wakati wa kufunga kikao kazi cha sekta ya utamaduni akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw. Raymond Mushi akizungumza na wadau wa utamaduni kuwapongeza kuwa na ushirikiano katika kutekeleza majukumu yao. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Utamaduni Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Afisa Bw. Habibu Msami
UT3 
Afisa Utamaduni kutoka Kiteto Bibi. Bihawa Masawika akitoa neno la shukrani wakati wa kufunga kikao kazi cha kumi cha sekta ya Utamaduni jana Jijini Dar es Salaam.
UT4 
Afisa Utamaduni kutoka Wilaya ya Mbogwe Mkoa wa Geita Bw. Athanas Michael akiimba shairi la kuhamasisha kudumisha Utamaduni wakati wa kufunga kikao kazi cha kumi cha sekta ya Utamaduni jana Jijini Dar es Salaam.
UT5 
Mshairi kutoka Chama cha Umoja wa Washairi Tanzania (UWASHATA) Bw. Issa Amiri Kilimo akiimba shairi la kuipongeza Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa kushirikiana na wadau wa utamaduni kuhamasisha masuala ya utamaduni wakati wa kufunga kikao kazi cha kumi cha sekta ya Utamaduni jana Jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Utamaduni washauriwa kutoiga tamaduni za nchi nyingine Wadau wa Utamaduni washauriwa kutoiga tamaduni za nchi nyingine Reviewed by crispaseve on 12:14 Rating: 5

No comments

Post AD