Header AD

WANAWAKE HAWA WAKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA WALIYOKUWA WAMEYAFICHA KATIKA NEPI WALIZOVAA UWANJA WA NDEGE WA JFK MAREKANI.

Woman Caught at JFK International with Cocaine Diaper Sentenced to Two Years in Prison

Wakati biashara ya usafirishaji wa madawa ya kulevya ikiwa imeshamiri hasa kwa nchi za Afrika na bara la Ulaya, wanawake wawili walikamatwa na katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa John F. Kennedy uliopo katika jiji la New York, maafisa wa usalama uwanjani hapo waliweza kubaina wadada hao ambao walikuwa wamefungusha takribani kilo 6.5 katika nepi walizokuwa wamezivaa, unga huo ambao ulikadiriwa kuwa na thamani ya dola za kimarekani 85,000 ulikuwa ukisafirishwa kutoka jamhuri ya Dominika kuingia New York Marekani ndipo wadada hao waliweza kubainika.

Taarifa za kipolisi zimedai kwamba wanawake hao waliweza kutambuliwa majina yao kupitia pasipoti zao kwa majina ya Michelle Blassingale(36) na Priscilla Pena, ndipo waliweza kubainika baada ya maafisa hao kuwakagua na kuhisi vitu vigumu katika nguo walizokuwa wamevaa,wadada hao wote walihukumiwa kwenda jela miaka miwili na faini licha kumtaja mtu aliyeapa mzigo huo ambaye alikuwa ni Raia wa Jamhuri ya Dominica kwa kuwalipa kiasi cha dola 8,000 kuweza kuingiza mzigo huo Marekani.
Woman Caught at JFK International with Cocaine Diaper Sentenced to Two Years in Prison
Pichani ni bi mdada Michelle Blassingale akionyesha jinsi walivyoufunga mzigo huo wa madawa ya kulevya katika nepi kisha kuivaa, sio mchezo aiseee
WANAWAKE HAWA WAKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA WALIYOKUWA WAMEYAFICHA KATIKA NEPI WALIZOVAA UWANJA WA NDEGE WA JFK MAREKANI. WANAWAKE HAWA WAKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA WALIYOKUWA WAMEYAFICHA KATIKA NEPI WALIZOVAA UWANJA WA NDEGE WA JFK MAREKANI. Reviewed by crispaseve on 23:42 Rating: 5

No comments

Post AD