Header AD

MASHABIKI 15 WAFARIKI DUNIA KWENYE MECHI YA TP MAZEMBE NA AS VITA NCHINI CONGO

TP Mazembe
Polisi wakiwarushia mabomu ya machozi mashabiki
Mashabiki 15 wa soka wamekufa kwa kukanyagana baada ya polisi kufyatua mabomu ya kutoa machozi kwenye kundi la watu kwenye uwanja wa soka  wa  Stempede uliopo katika jiji la Kinshasa, jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Kwa mujibu wa jeshi la  polisi nchini humo wamesema  mashabiki walipatwa na hasira jana jioni baada ya timu yao ya AS Vita Club kuchapwa kwa bao moja kwa sifuri na klabu ya Tp Mazembe toka mji wa Lubumbashi .
Majeruhi akipatiwa huduma ya kwanza na kikosi cha msalaba mwekundu
Kiongozi mmoja wa mjini huko ‘Emmanuel Akweti’ amesema askari polisi wanne walibughudhiwa na mashabiki na walipofyatua mabomu ya machozi ndipo mashabiki hao wakaanza kukimbia na kukanyagana hali iliyopelekea kusababisha vifo.
Aliongezea kwa kusema kuwa watu hao 15 wamekufa kwa kukosa hewa na wengine zaidi ya 24 wamejeruhiwa katika tukio hilo.
MASHABIKI 15 WAFARIKI DUNIA KWENYE MECHI YA TP MAZEMBE NA AS VITA NCHINI CONGO MASHABIKI 15 WAFARIKI DUNIA KWENYE MECHI YA TP MAZEMBE NA AS VITA NCHINI CONGO Reviewed by crispaseve on 06:40 Rating: 5

No comments

Post AD