Header AD

SHAVU LINGINE LANUKIA KWA RYAN GIGGS NDANI YA UNITED

Ryan GiggsMchezaji mkongwe wa klabu ya Manchester United ‘Ryan Giggs’ huenda akapata shavu la kuendelea kubaki katika benchi la ufundi kikosini hapo, baada ya kocha anayetarajia kujiunga na mashetani hao wekundu ‘Louis Van Gaal’ kuweka wazi kuwa anapenda kumuacha kocha mmoja aliyekuwa katika kikosi chake kipya kabla ya kujiunga na kuanza kazi rasmi.
Kocha huyo wa muda wa United hapo jana alishuhudia timu yake hiyo ikienda sare ya bao moja kwa moja na Southampton katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la St.Marys Stadium huku idadi kubwa ya mashabiki na wapenzi wa soka wakisubiria kuona uamuzi atakaotoa kocha huyo mdachi kuhusu hatma ya Giggs mara atakapodhibitishwa kuwa kocha wa United baadae wiki hii .
‘’Napojiunga na klabu mpya mara zote huwa nambakisha kocha mmoja kutoka benchi lililokuwepo, nikiwa Bayern nilimbakisha ‘Hermann Gerland’  ambaye sasa anafanya kazi na Pep Guardiolla’’ alisema Van Gaal ambaye kwa sasa anakinoa kikosi cha timu ya Taifa ya Uholanzi.
SHAVU LINGINE LANUKIA KWA RYAN GIGGS NDANI YA UNITED SHAVU LINGINE LANUKIA KWA RYAN GIGGS NDANI YA UNITED Reviewed by crispaseve on 06:53 Rating: 5

No comments

Post AD