Header AD

WAHAMIAJI 36 WAFA MAJI NA WENGINE 52 WAOKOLEWA KATIKA PWANI YA LIBYA


Wahamiaji 36 Libya
Wahamiaji walionusurika wakishuka katika boti ya uokoaji
Wahamiaji 36 wamekufa maji na wengine 52 wameokolewa baada ya boti yao kuzama katika pwani ya Libya ambayo inasemekana kuwa njia kuu ya wahamiaji wengi wanaojaribu kwenda Ulaya.
Mbali na wahamiaji waliokufa na kuokolewa, kuna wengine 54 ambao bado hawajaonekana baada ya wahamiaji walionusurika kusema kuwa boti ilikuwa na zaidi ya watu 130.
Mwishoni mwa wiki waziri wa Libya wa mambo ya ndani aliomba umoja wa Ulaya kufanya juhudi zaidi za kusaidia kupunguza wimbi la wahamiaji wanaopjaribu kwenda Ulaya kutafuta Maisha.
WAHAMIAJI 36 WAFA MAJI NA WENGINE 52 WAOKOLEWA KATIKA PWANI YA LIBYA WAHAMIAJI 36 WAFA MAJI NA WENGINE 52 WAOKOLEWA KATIKA PWANI YA LIBYA Reviewed by crispaseve on 06:45 Rating: 5

No comments

Post AD