Header AD

NGUMI ZILIVYOPIGWA MANZESE SIKU YA IDDI PILI



Kocha mkongwe wa mchezo wa masumbwi nchini Habibu Kinyogoli 'Masta' kulia akimvisha mkanda wa ubingwa bondia ramadhani Kumbele baada ya kumdunda Julius Kisalawe kwa point kushoto ni Refarii Ally Bakari.
Bondia Sadick Nuru kushoto akioneshana umwamba na Baraka Mchonge wakati wa mpambano wao ulifanyika Mazese Dar es salaam wakati wa sikukuu ya iddi pili Nuru alishinda kwa point mpambano huo .
Bondia Stevin Kobelo kushoto akirusha ngumi kumpiga Karim Ramadhani wakati wa mpambano wao uliofanyika siku ya iddi pili katika ukumbi wa Manyara park manzese Dar es salaam mpambano huo walitoka droo ya kufungana point.
Mabondia Joseph Gili kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Ibrahimu Tamba wakati wa mpambano wao uliofanyika siku ya Iddi pili katika ukumbi wa manyara park manzese Dar es salaam Tamba aklishinda kwa T.K.O  ya raundi ya nne.
Bondia Julius Kisalawe kushoto akipambana na Ramadhani Kumbele wajkati wa mpambano wao wa ubingwa wa TPBC uliofanyika siku ya Iddi pili katika ukumbi wa Manyara Park Manzese Dar es salaam Kumbele alishinda kwa point na kufanikiwa kuchukua ubingwa picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com.
NGUMI ZILIVYOPIGWA MANZESE SIKU YA IDDI PILI NGUMI ZILIVYOPIGWA MANZESE SIKU YA IDDI PILI Reviewed by crispaseve on 01:59 Rating: 5

No comments

Post AD