NGUMI ZILIVYOPIGWA MANZESE SIKU YA IDDI PILI
Kocha mkongwe wa mchezo wa masumbwi
nchini Habibu Kinyogoli 'Masta' kulia akimvisha mkanda wa ubingwa bondia
ramadhani Kumbele baada ya kumdunda Julius Kisalawe kwa point kushoto
ni Refarii Ally Bakari.
Bondia Sadick Nuru kushoto akioneshana umwamba na Baraka Mchonge wakati wa mpambano wao ulifanyika Mazese Dar es salaam wakati wa sikukuu ya iddi pili Nuru alishinda kwa point mpambano huo . |
Bondia Stevin
Kobelo kushoto akirusha ngumi kumpiga Karim Ramadhani wakati wa
mpambano wao uliofanyika siku ya iddi pili katika ukumbi wa Manyara park
manzese Dar es salaam mpambano huo walitoka droo ya kufungana point.
Mabondia Joseph Gili kushoto
akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Ibrahimu Tamba wakati wa
mpambano wao uliofanyika siku ya Iddi pili katika ukumbi wa manyara park
manzese Dar es salaam Tamba aklishinda kwa T.K.O ya raundi ya nne.
Bondia Julius Kisalawe kushoto
akipambana na Ramadhani Kumbele wajkati wa mpambano wao wa ubingwa wa
TPBC uliofanyika siku ya Iddi pili katika ukumbi wa Manyara Park Manzese
Dar es salaam Kumbele alishinda kwa point na kufanikiwa kuchukua
ubingwa picha na www.superdboxingcoach. blogspot.com.
NGUMI ZILIVYOPIGWA MANZESE SIKU YA IDDI PILI
Reviewed by crispaseve
on
01:59
Rating:
Post a Comment