UGANDA YAFUTA SHERIA DHIDI YA USHOGA
Taswira za waliokuwa wakipinga sheria dhidi ya ushoga nchini Uganda.
MAHAKAMA
ya kikatiba nchini Uganda imefutilia mbali sheria dhidi ya wapenzi wa
jinsia moja ambayo ilisababisha mataifa ya magharibi kuinyima msaada.
Kadhalika
sheria hiyo ilizua gumzo sana siyo tu Uganda bali duniani kote ambapo
mataifa ya magharibi yalilazimika kuingilia kati.
Mahakama
ilisema kuwa mswada huo kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria ulipitishwa
na wabunge ambao idadi yao haikutosha kupitisha mswada hivyo ni kinyume
na sheria.
Vitendo
vya mapenzi ya jinsia moja, tayari vilikuwa vimeharamishwa nchini
Uganda, lakini sheria hiyo mpya pia iliharamisha hatua zozote za kueneza
mapenzi ya jinsia moja na wakati huu hata kuwajumuisha wanawake
wasagaji kama sehemu ya wapenzi wa jinsia moja.
Mataifa kadhaa ya magharibi yamesitisha msaada kwa Uganda hasa baada ya sheria hiyo mpya kupitishwa.
Chanzo: BBCSWAHILI
UGANDA YAFUTA SHERIA DHIDI YA USHOGA
Reviewed by crispaseve
on
09:23
Rating:
Post a Comment