WAZIRI MKUU ATAKA VITA DHIDI YA UJANGILI IWE YA PAMOJA

Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya
Waziri Mkuu, Aggrey Mwanri mara baada ya kuwasili kwenye makao makuu ya
jumuiya ya Afrika Mashariki kufunga Mkutano wa kupiga vita dhidi
ujangili wa wanyamapori na kuendeleza uhifadhi wa wanayamapori mjini
Arusha Novemba 8, 2014. Kushoto ni Waziri wa Mali asili na utalii Mh.
Lazaro Nyalandu na wa pili kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa
Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu.(Picha zote na Zainul Mzige
wa MOblog
--
* Ataka iundwe timu kufuatilia utekelezaji wa Azimio la Arusha 2014
Na Ofisi ya Waziri Mkuu
WAZIRI
MKUU Mizengo Pinda amesema inahitajika dhamira ya kweli kutoka kwa
wadau wote katika kutekeleza Azimio la Arusha la kukabiliana na ujangili
na kuendeleza hifadhi za wanyama katika nchi za Afrika Mashariki na
zilizo Kusini mwa Ikweta.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana jioni (Jumamosi, Novemba 8, 2014) mara
baada ya kufunga mkutano wa kikanda wa siku mbili uliojadili mbinu za
kupambana na biashara haramu ya wanyamapori ulioandaliwa na Wizara ya
Maliasili na Utalii jijini Arusha, Waziri Mkuu alisema: “Suala hili
linataka uwajibikaji wa pamoja. Mashirika na taasisi, wananchi na
viongozi sote kama wadau wakuu, kila mmoja anapaswa kushiriki vita hii
kama kweli tunataka tuitokomeze.”
WAZIRI MKUU ATAKA VITA DHIDI YA UJANGILI IWE YA PAMOJA
Reviewed by crispaseve
on
00:08
Rating:
Post a Comment